NAGU:Wananchi shirikianeni kutunza Miradi ya maendeleo


Ili kuhakikisha miradi ya maendeleo inadumu,Wananchi wa kata ya Endagaw Wilayani Hanang’ mkoani Manyara wametakiwa kushirikiana kwa pamoja katika kuitunza  ili iweze kuwasaidia sasa na hata
vizazi  vijavyo. 

Mbunge wa Jimbo la Hanang’  Dkt. Mary  Nagu ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara
uliofanyika  katika kijiji cha moram  Kata  ya Endagaw ambapo amesema kuwa ni vema wananchi wakatambua kuwa miradi hiyo  imetumia gharama kubwa  na ni kwa manufaa yao .

 Amesema kwamba ujenzi wa soko la mazao la kimataifa lililopo
 katika kata  hiyo umekamika hivyo ni lazima waweke
 mfumo madhubuti wa soko hilo ili kuweza kuleta manufaa kwa
 wananchi wa Wilaya  hiyo.

Ndugu zangu  ujenzi wa soko letu la Kimataifa umekamilika na soko ni mfumo, ni lazima tuweke mfumo madhubuti wa kuendesha soko lile ili liweze kutusaidia, bila kufanya hivyo tutajikuta tunashindwa kunufaisha  wana Hanang’  na badala yake watanufaika watu wa kutoka nje ya  hapa’’ Alieleza Dkt.  Nagu.

Alisema kuwa soko hilo litawaweka pamoja  wananchi waKata ya Endagaw na Hanang’ kwa ujumla ambapo wao ndio wataamua  kuuza mazao yao kwa bei ya  kimataifakwa kuwa ni soko la kimataifa,  si kama ilivyo sasa  ya kupangiwa bei na wanunuzi.

Aidha alisema  kwamba ni lazima viongozi wawekemfumo  madhubuti wa  kuwaletea vijana maendeleo kwa kuwapatia ajira katika  soko hilo na hiyo itasaidia  kufanyika shughuli za kiuchumi  katika wilaya yao na uchumi wao utaimarika maradufu.

Kwa upande wa mradi wa umwagiliaji, Mhe: Nagu alisema kuwa  Nchi haina  uhakika wa mvua  za kutosha hivyo ni miradi ya umwagiliaji tu ndio itawahakikishia chakula  cha kutosha na mazao ya biashashara.

‘Ninaomba  muwe na  mpangilio mzuri ili  manufaa yawe makubwa na muangalie tija  ya maeneo 
 ya umwagiliaji kwa kupangilia mazao ya kulima katika maeneohayo’’ Alisisitiza Nagu. 

Naye Mtendaji wa Kata ya Endagaw Bw. Yusuph Jackson alisema kuwa ujenzi wa soko  la mazao la kisasa ambalo limekamilika na hivyo wanaomba kufunguliwa  mapema  ili wananchi waweze kuuza mazao yao na kufaidika na ujenzi wa soko hilo katika kata yao.

No comments