Rais wa Uturuki ahutubia Bunge

Rais wa UTURUKI, RECEP TAYYIP ERDOGAN amelihutubia bunge la nchi hiyo
kwa mara ya kwanza baada ya jaribio la kuipindua serikali yake kushindwa na
kulaumu baadhi ya watu wanaosema utawala wake ni wa kidikteta.

Rais ERDOGAN amesema serikali yake kupitia Wizara ya Mambo ya Nje,
itaonesha picha za video na mnato kote duniani zinazoonesha matukio ya
uvamizi katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo, ili kuonesha ushahidi wa
namna serikali yake isivyo na utawala wa kidikteta.

Zaidi ya watu Elfu hamsini wamewekwa kizuizini na wengine kufukuzwa kazi
baada ya jaribio hilo kushindwa


No comments