Thursday, 28 April 2016 Mwili wa Papa Wemba wawasili DRC
Mamia ya watu wamekongamana nje ya uwanja wa ndege wa Kinshasa
kuupokea mwili wa mwanamuziki Papa Wemba uliowasili nchini humo kutoka
Abidjan
Mwanamuziki huyo ambaye ametajwa kuwa mmoja ya waanzilishi wa muziki
wa kizazi kipya cha Soukous anatarajiwa kuzikwa siku ya Jumanne baada ya
mwili huo kuwekwa katika uwanja wa mpira kwa raia kutoa heshima zao za
mwisho.
Maafisa wa serikali na wanadiplomasia watahudhuria ibada ya kumkumbuka
mwanamuziki huyo katika uwanja wa ndege kabla ya mwili huo kupelekwa
katika chumba cha kuhifadhia maiti.
Tamasha la bure la usiku kucha lilifanyika mjini Abidjan ambapo mwanamuziki
huyo alianguka alipokuwa akiimba.Mwanahabari wa BBC Tamasin Ford
anasema kuwa mashabiki wengi walivalia nguo nyeusi na kubeba mishumaa ili
kutoa heshima kwa nguli huyo wa muziki.
Mkewe Papa Wemba na wasaidizi wake pia walikuwepo.
No comments