Mkurugenzi Bagamoyo afutwa kazi

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Azimina Mbilinyi
ametumbuliwa na Rais John Magufuli baada ya kufanya kazi kwa siku 24 tangu
ateuliwe.

Azimina ambaye aliteuliwa Julai 7 mwaka huu uteuzi wake umetenguliwa na Dk
Magufuli kwa kutoridhishwa na utendaji wake wa kazi.
Kutenguliwa huko kulifanyika jana kwa mujibu wa barua iliyotolewa na Katibu
Mkuu wa Ofisi ya Rais(Tamisemi), Musa Iyombe.

No comments