IS wadai kuhusika shambulizi la Nice
Kundi la wapiganaji wa Islamic State limedai kuwa shambulio lililofanywa na
mtu aliyewakanyaga watu na lori alikuwa mmoja wa wanachama wake.
Madai hayo yameonekana kwenye mtandao wa kundi hilo unaojulikana kama
Amaq.
IS wamekuwa wakitumia mtandao huo kueneza propaganda zao.
Hata hivyo hakuna habari za kuthibitisha kuwa kundi hilo lilihusika moja kwa
moja na shambulio hilo.
Tovuti hiyo ya Amaq imekuwa ikieneza taarifa ya IS inayohimiza waislamu
kushambulia mtu au watu wanaotoka nchi za muungano wa mataifa
yanayoshambulia kundi hilo.
Hata hivyo kuna wanaosema IS imetumia nafasi ya shambulio hilo kujikuza
ingawa huenda kamwe hawakuhusika.
*BBC*

No comments