Thursday, April 28, 2016 Vipaza Sauti Vya Bunge Vyaharibika, Bunge Lasimama kwa Dakika 30

Shughuli za Bunge la Muungano leo zilisimama kwa dakika 30 kabla ya
kuendelea tena, baada ya vipasa sauti vya ukumbini kushindwa kufanya
kazi

Spika wa Bunge, Job Ndugai amelazimika kuahirisha shughuli mara
baada ya kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu
ambacho hata hivyo wabunge walichukua muda mrefu kuuliza maswali
kutokana na kuhama hama wakitafuta mahali pa kusikika.

Awali, wabunge waliokuwa na nafasi ya kuuliza maswali walilazimka
kuhama maeneo yao na kuzua minong’ono ndani ya ukumbi, huku
Mbunge wa Mkuranga (CCM), Abdallah Ulega na Mbunge wa Manonga
(CCM), Seif Gulamali wakilazimika kuuliza maswali yao wakiwa uso kwa
uso na Waziri Mkuu mbele ya ukumbi.

Hata hivyo, kuna hali ya sintofahamu, kwani vipaza sauti vimeharibika
ikiwa ukumbi huo umefanya kazi kwa siku sita tu tangu ulipokabidhiwa
baada ya ukarabati mkubwa.

April 18, Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson alikabidhiwa ukumbi
huo ikielezwa kuwa ulikuwa umefanyiwa matengenezo makubwa katika
maeneo mbalimbali kwa lengo la kuuboresha.

No comments