Mahakama ya wilaya ya Mpanda yamuachia huru Laurence Masha
Mahakama ya Wilaya, Mpanda imemuachia huru Lawrence Kego Masha
aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Nyamagana Mwanza
pamoja na washtakiwa wengi ambao ni Viongozi wa Chadema Jimbo la
Nsimbo, Katavi katika makosa mawili ya Kula Njama Ili Kutenda Kosa na
Kuhutubia Wakimbizi wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2015 na kosa lingine la
kuingia makazi ya Wakimbizi bila Kibali.
Mahakama imesema kwamba upande wa mwendesha mashtaka umeshindwa
kutoa ushahidi wowote unaonyesha kwamba washtakiwa hao walikutana na
kupanga njama kutenda kosa.
Pia hakuna ushahidi wowote kuonyesha kwamba washtakiwa walikamatwa
wakihutubia wakimbizi.
Ila Mahakama iliona kwamba washtakiwa hao wana kosa la kujibu kwa shtaka
la kuingia kwenye kambi/makazi ya wakimbizi bila kibali.
Mara baada ya uamuzi huo washtakiwa walitakiwa kutoa utetezi wao ambapo
washtakiwa Lawrence Masha na Stansalaus Kaswele walitoa utetezi
wakiongozwa na Wakili Albert Msando.
Leo Mahakama imetoa hukumu na kusema kwamba washtakiwa wote saba
No comments