Upinzani DRC waanzisha kampeni ya "Kwaheri Kabila"

Zaidi ya vyama kumi vya upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
vimeungana kuanzisha kampeni ya kumshinikiza Rais Joseph Kabila
kuondoka baada ya muda wake kukamilika mnamo tarehe 20 Disemba.
Kampeni hiyo iliyopewa jina la "Kwaheri Kabila" inamtaka rais huyo
anayeshutumiwa kwa kuchelewesha chaguzi, kuondoka madarakani bila ya
masharti yoyote na kutangaza waziwazi kuwa hatong'angania madaraka.
No comments