MAREHEMU SAMWELI SITTA APUMZISHWA KATIKA NYUMBA YAKE YA MILELE,WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AONGOZA WAOMBOLEZAJI

November 12 2016 yamefanyika mazishi ya Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samuel John Sitta aliyefariki dunia November 7 2016 katika hospitali ya Technical University of Munich nchini Ujerumani.
Mazishi hayo yamefanyika Urambo Tabora kwenye eneo la makaburi ya ukoo wa Sitta ambayo yapo takribani km 2 kutoka nyumbani kwake.
Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa na Mkewe Mary wakweka shada la maua kwenye kaburi la Spika Mstaafu Samuel Sitta yaliyofanyika Urambo Novemba 12, 2016.
Waziri Mkuu, Kasim Majliwa na mkewe Mary wakitupa udongo kwenye kaburi la Spika Mstaafu, Samuel Sitta katika mazishi yaliyofanyika Urambo, Novemba 12, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments