Mfanyabiashara Mtanzania mwenye asili ya Asia amamepandishwa kizimbani kwa kuhujumu uchumi kwa njia ya mitandao

Image result for logo ya mahakamaImage result for logo ya mahakama

Na.Vero Ignatus ,Arusha.







Mtanzania mwenye asili ya Asia Firoz Khan, amepandishwa mahakama ya Hakimu Mkazi jijini Arusha kujibu mashtaka ya kuingiza mtambo wa mawasiliano na kufanya utapeli kupitia njia ya mawasiliano


Awali, Akisomewa mashtaka hayo na wakili wa Serikali  Johovanes Zacharia alisema mshtakiwa huyo anakabiliwa na makosa 7 ya kufanya udanganyifu wa mitandao uliopelekea kuliingizia taifa hasara ya 600 milioni.


Akitaja makosa  hayo alisema ni pamoja na kuingiza mtambo wa mawasiliano bila kibali,kutengeneza njia ya mawasiliano kwaajili ya kukwepa tozo za mawasiliano ndani na nje ya nchi, kutumia mtambo huo kinyume na sheria ya mawasiliano, kufanya udanganyifu wa kujinufaisha  za nje, kujifanya ni wakala wa usajili wa laini za simu bila kutambulika, kusajili watu wasitambulika


Awali wakili huyo aliiambia mahakama kuwa mtuhumiwa huyo alitenda makosa hayo mnamo mwezi wa Tatu na aprili mwaka jana  na kuachiwa kwa dhamana kutokana na sababu ambazo zimempa mamlaka Mkurugenzi wa mashtaka mahakama imemuondolea kesi mbili na kumfungulia upya tena kesi  huku ikiweka pingamizi ya dhamana ya mtuhumiwa huyo


"Mkurugenzi wa mashtaka ametoa hati ya kumnyima dhamana mtuhumiwa na imewasilishwa mahakamani tayari,"alisema Johovanes.


Upande wa wakili wa utetezi wa mtuhumiwa huyo, aliiomba mahakama impe dhamana mteja wake kutokana na kushtakiwa kwa kosa linalofanana kama hilo kwa  kwa mara pili.


Pia alisema, mteja wake anahaki ya kupwa dhamana kwakua Mkurugenzi wa makosa ya jinai alishindwa kuonesha sababu zitakazomnyima dhamana mtuhumiwa huyo


"DPP hajaonesha sababu kuwa ni ni madhara yapi yako kwa mtuhumiwa akiwepa dhamana au itaathiri vip kesi hiyo akiwa nje kwa dhamana.

"Sielewi ni kwanini mtuhumiwa anafunguliwa kesi, inafungwa halafu imefunguliwa tena"alisema wakili wa mshatakiwa.
Kwa upande wake mwanasheria wa mamlaka ya mawasiliani TCRA amesema kuwa mtu yeyote yule atakayetumia mitandao vibaya sheria itachukua mkondo wake.

No comments