Samia Suluhu:Nchi za Afrika zatakiwa kuruhusu watu binafsi na mashirika binafsi kupeleka kesi mahakama ya Afrika

 Image result for mama samia suluhu
 Makamu wa rais Samia Suluhu

Na Vero Ignatus Arusha 

Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania   Samia Suluhu, amezitaka nchi zilizosaini mkataba wa kulinda na kutetea haki za kibinadamu ziruhusu watu binafsi na mashirika binafsi kupeleka kesi mahakama ya Afrika.
 
Amezungumza hayo wakati akifungua mkutano wa 5 wa demokrasia, haki za binadamu na utawala bora, amesema ni wakati sasa wa nchi hizo kuiga mfano kutoka nchi ya Tanzania kwa kuwaruhusu wananchi wake pamoja na mashirika binafsi kufungua kesi kwenye mahakama ya afrika 

Awali, amesema licha ya Afrika kuanza kuwa na muitikio mkubwa kwenye maswala ya utetezi wa haki za kibinadamu, kwa nchi ya Tanzania imekuwa mstari wa mbele kuitikia matamko pamoja na kuyatekeleza maswala ya haki za kibinadamu kutoka kiwango cha mataifa hadi kufikia wananchi.
.
"Tumefungua taasisi na vyombo mbalimbali vinavyoshughulia utetezi wa haki hasa haki za binadamu, haki za wanawake na haki za watoto na tumehakikisha kuwa kila mwananchi haki zake za msingi anazipata na kuzilinda, "alisema Samia Suluhu
"Kwasasa tumehakikisha watu wote wanapata haki ya elimu, ndio mana kuna elimu bure, haki ya maisha, haki ya kupata makazi, 

Kwa upande wa haki ya Afya, alisema Tanzania ipo katika mchakato wa kuongeza bajeti yake kufikia 10%, ikiwa ni kuitikia amri ya tamko la Abuja lililotaka bajeti ya Afya kwa nchi za Afrika ifike asilimia 15%

Pia amesema licha ya Tanzania kufanya vizuri kwenye utetezi na ulindaji wa haki zawanamke pamoja na kumuwezesha kushiriki kwenye ngazi zote za maamuzi,idadi ya ushirikishwaji wa wanawake kwenye bodi za maamuzi kwenye sekta binafsi bado ni changamoto
"Kwasasa kuna benki ya wanawake inayotoa mikopo kwa wanawake kwaajili ya kuwawezesha kiuchumi, naomba nitoe wito kwa benki binafsi zitenge pesa wanawake kwaajili ya kuwakopesha, "alisema Suluhu
Kwa Upande wa jaji Mkuu wa nchi, Othman Chande, alisema kitendo cha Tanzania kuwa miongoni mwa nchi 7 zilizoruhusu, wananchi kifungu kesi na mahakama ya Afrika, watanzania wengi wamejitokeza kufungua kesi kwenye mahakama hiyo 

" Kuruhusu wananchi kufungua kesi kwenye mahakama ya Afrika ni moja ya chachu ya kusaidia utekelezaji wa haki za kibinadamu, "alisema Jaji Chande
Rais wa Mahakama ya Afrika Silvia Ore, pia alisema kuruhusu kufungua kesi kwenye mahakama hiyo si mbaya kwakua ni moja ya mikakati ya kuhakiki haki za kibinadamu zinalindwa na kutetea.

No comments