Lema ameshindwa kufikishwa mahakamani kutokana na sababu zisizojulikana
Pichani Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema na mkewe
Na.Vero Ignatus, Arusha
Mbunge
wa Arusha mjini Godbless Lema ambaye yuko mahabusu ya magereza ya
kisongo kwa kukosa dhamana kutokana na kukabiliwa na kesi mbili za
jinai, ameshindwa kufikishwa
Mbunge
wa Arusha mjini Godbless Lema ambaye yuko mahabusu ya magereza ya
kisongo kwa kukosa dhamana kutokana na kukabiliwa na kesi mbili za
jinai, ameshindwa kufikishwa mahakamani kutokana na sababu
zisizojulikana
Kesi hiyo ni kesi nyingine
ambayo ilipangwa kuanza kusikilizwa jana akiwa anashtakiwa yeye pamoja
na mke wake kwa kosa la kumtukana mkuu wa Mkoa wa Arusha ,Mrisho Gambo
,pamoja na kufanya uchochezi
Akiambia mahakama
,mbele ya hakimu mkazi Augustino Rwezile , wakili wa serikali
,Fortunatus Mhale ,alisema kushindwa kufikishwa mahakamani kwa mbunge
huyo ni kutokana na sababu za kimazingira hivyo aliomba tarehe ipangwe
kwaajili ya kusikilizwa kwa hoja ya awali ya kesi hiyo
Pia
,alisema upande wa Jamhuri hakuwa na makosa kutokana na hati hiyo ya
kuletwa mahakamani ilitakiwa itoke mahakamani kwenda magereza na si
kutoka upande wa jamhuri kwenda gerezani
"Nadhani
wakili wa tetezi anachanganya ,si upande wa jamhuri ambao
hawakutekeleza amri hiyo bali ni magereza ndio ambao hawajatekeleza amri
hiyo ,"Alisema wakili Fortunatus
Pia kutokana
na upande wa utetezi wa mshtakiwa kutaka ,upande wa jamhuri kupewa
adhabu kwa kudharau mahakama,wakili huyo ,aliiambia mahakama adhabu hiyo
ilipaswa kutolewa kwa magereza na si kwa upande wa jamuhuri kwakua
magereza ilipaswa kutekeleza amri hiyo
Hata
hivyo ,alisema yeye yuko kwaajili ya kumuwakilisha mkurugenzi wa
mashtaka (DPP) na si upande wa gereza hivyo alitaka hati hiyo ya
kumleta mahakamani iltolewe ili aweze kusomewa hoja za awali
"Upelelezi umekamilika naomba tarehe ya kusikiliza hoja ya awali itolewe ,"Alisema Fortunatus
Uande
wa Utetezi ,wakili John Malya ,aliendelea kuitaka upande wa jamhuri
iambie mahakama sababu kamili ni zipi zilizopelekea mbunge huyo
kushindwa kufikishwa mahakamani
Pia kutokana
na kuwepo kwa mvutano dhidi ya jamuhuri na upande wa utetezi ,aliomba
mahakama ipange siku ya leo kusikilizwa kwa kesi hiyo ,ilikuepusha
muingiliano wa kesi nyingine ambazo zilikuwa zinamkabili mbunge huyo
Kutokana
na ombi hilo ,Hakimu Mkazi Rwegizile ,alikubali na kutoa amri ya hati
ya kumleta mahakamani mbunge huyo itolewe na mwendesha mashtaka na
aletwe mapema asubuhi kwaajili ya kusomewa hoja za awali za kesi hiyo
Mbunge
wa arusha Mjini,Godbless Lema yuko mahabusu kutokana na kukosa
dhamana,kutokana na kukabiliwa na kesi ya jinai ya kufanya uchochezi
akiwa kwenye mikutano yake ya hadhara kuwa ameoneshwa kama rais Magufuli
hatojirekebisha atakufa kabla ya 2020 ,lakini pia yeye na mke wake
wanakabiliwa na kesi nyingine ya kumutita Mkuu wa Mkoa Mrisho Gambo
"Shoga "Ambako Mke wake alisema alimuita shoga mbunge huyo kuwa ni
rafiki yake na si kama alivyochukulia mkuu huyo wa mkoa
Kesi hiyo ni kesi nyingine
ambayo ilipangwa kuanza kusikilizwa jana akiwa anashtakiwa yeye pamoja
na mke wake kwa kosa la kumtukana mkuu wa Mkoa wa Arusha ,Mrisho Gambo
,pamoja na kufanya uchochezi
Akiambia mahakama
,mbele ya hakimu mkazi Augustino Rwezile , wakili wa serikali
,Fortunatus Mhale ,alisema kushindwa kufikishwa mahakamani kwa mbunge
huyo ni kutokana na sababu za kimazingira hivyo aliomba tarehe ipangwe
kwaajili ya kusikilizwa kwa hoja ya awali ya kesi hiyo
Pia
,alisema upande wa Jamhuri hakuwa na makosa kutokana na hati hiyo ya
kuletwa mahakamani ilitakiwa itoke mahakamani kwenda magereza na si
kutoka upande wa jamhuri kwenda gerezani
"Nadhani
wakili wa tetezi anachanganya ,si upande wa jamhuri ambao
hawakutekeleza amri hiyo bali ni magereza ndio ambao hawajatekeleza amri
hiyo ,"Alisema wakili Fortunatus
Pia kutokana
na upande wa utetezi wa mshtakiwa kutaka ,upande wa jamhuri kupewa
adhabu kwa kudharau mahakama,wakili huyo ,aliiambia mahakama adhabu hiyo
ilipaswa kutolewa kwa magereza na si kwa upande wa jamuhuri kwakua
magereza ilipaswa kutekeleza amri hiyo
Hata
hivyo ,alisema yeye yuko kwaajili ya kumuwakilisha mkurugenzi wa
mashtaka (DPP) na si upande wa gereza hivyo alitaka hati hiyo ya
kumleta mahakamani iltolewe ili aweze kusomewa hoja za awali
"Upelelezi umekamilika naomba tarehe ya kusikiliza hoja ya awali itolewe ,"Alisema Fortunatus
Uande
wa Utetezi ,wakili John Malya ,aliendelea kuitaka upande wa jamhuri
iambie mahakama sababu kamili ni zipi zilizopelekea mbunge huyo
kushindwa kufikishwa mahakamani
Pia kutokana
na kuwepo kwa mvutano dhidi ya jamuhuri na upande wa utetezi ,aliomba
mahakama ipange siku ya leo kusikilizwa kwa kesi hiyo ,ilikuepusha
muingiliano wa kesi nyingine ambazo zilikuwa zinamkabili mbunge huyo
Kutokana
na ombi hilo ,Hakimu Mkazi Rwegizile ,alikubali na kutoa amri ya hati
ya kumleta mahakamani mbunge huyo itolewe na mwendesha mashtaka na
aletwe mapema asubuhi kwaajili ya kusomewa hoja za awali za kesi hiyo
Mbunge
wa arusha Mjini,Godbless Lema yuko mahabusu kutokana na kukosa
dhamana,kutokana na kukabiliwa na kesi ya jinai ya kufanya uchochezi
akiwa kwenye mikutano yake ya hadhara kuwa ameoneshwa kama rais Magufuli
hatojirekebisha atakufa kabla ya 2020 ,lakini pia yeye na mke wake
wanakabiliwa na kesi nyingine ya kumuita Mkuu wa Mkoa Mrisho Gambo
"Shoga "Ambapo Mke wake alisema alimuita shoga mbunge huyo kuwa ni
rafiki yake na si kama alivyochukulia mkuu huyo wa mkoa
No comments