Jumatano.4 APRIL 2016.TFDA YATOA MAFUNZO YA SIKU MOJA KWA WAHARIRI NA WAANDISHI WA VYOMBO MBALIMBALI VYA HABARI MKOANI ARUSHA JUU YA MAJUKUMU YA TFDA.

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA)Imetoa mafunzo ya siku moja kwa wahariri na waandishi wa habari mkoani Arusha,Huku malengo ya mafunzo hayo yakiwa na lengo la kuifahamisha jamii kupitia waandishi kuhusu majukumu ya TFDA.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi mkuu wa Tfda, Mkurugenzi wa Huduma ya mahabara Bi Charys Ugullum amesema kuwa jukumu kubwa walilo nalo Mamlaka ya chakula.na dawa ni kuhakikisaha kuwa, kuhamashisha wadau kuhusu sheria ya kudhibiti ubora na usalama wa chakula,dawa,vipodozi na vifaa tiba na iuweka mikakati ya pamoja ya namna ya kuisimamia na kuitekeleza.

Aidha bi Charys amesema kuwa tokea kuanzishwa kwa (TFDA) Julai 2003 tayari mamlaka hiyo imeshasajili bidhaa 39,596 za chakula ,dawa,vipodozi na vifaa tiba nchini huku idadi hii ikiwa inaongezeka mwaka hadi mwaka,mahalani,kutoka bidhaa 2,357 zilizosajiliwa mwaka 2005 hadi kufikia idadi tajwa kwa sasa.

Mkurugenzi wa Huduma ya Mahabara (TFDA) Bi Charys Ugullum akiwa anatoa ufafanuzi juu ya majukumu na Kazi za TFDA, Kwa Wahariri na Waandishi wa vyombo mbalimbali vya Habari jana Mkoani Arusha.

Bi Charys amesema kuwa pamoja na changamoto za udhibiti,TFDA pia imeweza kupata hati safi kwenye hesabu na vitabu vya mamlaka kwa kipindi cha miaka 12 mfululizo tangu kuanzishawa 2003,Utoaji huduma kwa kiwango cha kimataifa ISO 9001:2015,Mahabara kutambulika na Shirika la Afya Duniani (WHO)Pamoja na mahabara ya Chakula na Microbiolojia kupata cheti cha umahiri cha ISO/IEC 17025:2005 ambavyo vyeti hivyo vimeshikiliwa na TFDA hadi sasa.

Naye mgeni rasmi katika Mafunzo hayo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Daudi Filex Ntibenda,amesema kuwa (TFDA )haiwezi kufanya kazi peke yake bila kuwa na wadau wa kutoa elimu kwa jamii ambao ni waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali,na ameongeza kuwa majukumu ya msingi ya Taasisi hii ni ni kuhakikisha afya ya Wananchi inalindwa,pamoja.na kutoa elimu kwa umma,mara kwa mara ili.kuhakikisha kuwa wanapata taarifa sahihi juu ya bidhaa zilizopo katika soko ili waweze kufanya maamuzi sahihi kabla ya kuzitumia.

Ntibenda amesema kuwa suala la elimu kwa umma kuhusu udhibiti wa bidhaa , chakula,dawa,vipodozi na vifaa tiba ni endelevu na linahitaji mikakati tofauti tofauti ikiwa ni pamoja na ushirikishwaji wa wadau mbalimbali,kwani changamoto kubwa ni uwepo wa duni na bandia katika soko sanjari na matangazo ya bidhaa hususani dawa na vipodozi vilivyopigwa marufuku na Serikali kutokana kuwa na viambata SUMU kwa watumiaji amesema kuwa.matangazo haya yamekuwa yakirushwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari na Mitandao ya kijamiibila ya kuwa na kibali cha TFDA,na matakwa ya Sheria na Kanuni na hivyo kuchangia kupotosha jamii.


Mkuu wa Mkoa Wa Arusha Daud Filex Ntibenda.



Wahariri na waandishi wahabari wakiwa wakiwa katika mafunzo Mkoani Arusha.
Katika picha ya pamoja.

Meneja wa TFDA Mkoa wa Arusha Denis Matiko Akizungumza na Wahariri pamoja na waandishi wa habari.

No comments