Mbaroni Kwa Kukutwa Wakitoa Mamilioni Kwa ATM Za Watu 19





Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za
kukamatwa wakiwa wanatoa fedha benki ya NMB tawi la Mpanda kiasi cha
shilingi 3,680,000 wakiwa na kadi za ATM 19 mali za watu tofauti pamoja na
namba za siri za kadi hizo. .

Kaimu Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Katavi Damasi Nyanda amesema
watuhumiwa hao watatu walikamatwa jana majira ya saa tatu usiku katika
Tawi la NMB Mpanda .
Watuhumiwa hao ambao majina yao yamehifadhiwa kwa kuwa upelelezi bado
unaendelea, wamekamatwa na askari wa jeshi la polisi waliokuwa wakilinda
Benki hiyo.

Nyanda ameeleza kuwa watumiwa walikamatwa baada ya askari polisi
kuwatilia mashaka kutokana na kuwaona wakiwa wamekaa muda mrefu kwenye
chumba cha mashine ya kutolea fedha .

Amesema baada ya kuwatilia mashaka polisi waliingia ndani ya chumba hicho
na kuwakuta watuhumiwa hao wakiwa wanaendelea kutoa fedha katika mashine
tatu zilizomo kwenye mashine za kutolea fedha.

Kaimu Kamanda alieleza ndipo askari polisi walipoamua kuwapekua
watuhumiwa na waliwakuta wakiwa na kadi za ATM 19 mali za watu tofauti
pamoja na namba za siri za kadi h izo na walikuwa tayari wameishatoa kiasi
cha fedha taslimu shilingi 3,680,000.

Amezitaja Namba za Kadi za ATM walizokamatwa nazo watuhumiwa kuwa ni
AC 61908000058,AC 61902403196,AC61902400417,AC61908000427,AC
61902240100,AC 61908000237, AC 61902400518 AC 61910000645, AC
61910004240,AC 61908000609 AC 61902403168

Kaimu kamanda Nyanda amezitaja kadi za ATM zingine zilizokamatwa kuwa ni
zenye namba AC 61910000537,AC 61902402653, AC 61910000250, Ac
61902400818, AC 61908000449,AC1902403219 AC 61910002329 na AC
70408100131.

Amesema watuhumiwa wanatarajia kufikishwa mahakamani baada ya
uchunguzi wa tukio hilo kukamilika na bado watuhumiwa wote watatu
wanaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano zaidi .

Kaimu kamanda ametoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kutoa siri kwa
watu za namba zao za siri za kadi wanazozitumia kwenye ATM za benki .

No comments