Olemeiseiyeki:Tozo kubwa ni Kero kwa Utalii Tanzania.




Mbunge wa Arumeru Magharibi Gibson Olemeiyeseki.

Na Vero Ignatus Arusha.

Serikali  imetakiwa kufungua ofisi za utalii katika kila nchi  ambazo zinaleta watalii hapa nchini pamoja na kupunguza viingilio vya wageni wanaotembelea hifadhi zetu za taifa ili kuweza kuongeza idadi ya watalii wanaoingia hapa nchini  .

Hayo yamesemwa na Mbunge wa jimbo la Arumeru magharibi  Gibson Olemeiseyeki wakati  akiongea na waandishi wa habari alipotembelea katika maonyesho ya utalii ya Karibu fair yanayofanyika ndani ya viwanja ya magereza nje vilivyopo ndani ya jiji la Arusha .

Amesema kuwa  serekali inapaswa kufungua ofisi katika kila  nchi ambazo zinaleta wageni hapa nchini ili kuweza kutangaza utalii wetu vizuri,na ili kuweza kupata wageni wengi zaidi  ambapo wakiingia kwa wingi watasaidia kuongeza pato la taifa na kupunguza tatizo la ajira kwani vijana.

Mbunge huyo amesema  kuwa ni jambo la ajabu nchi kama Tanzania ambayo inavivutio vingi vya utalii , hukubikishika nafasi ya  kumi bora ambazo zinaongoza kwa kuwa na vivutio vya utalii lakini ni nchi ambayo inaongiza watalii wachache sana ukilinganisha na vivutio vilivyopo,kwa mwaka mzima inapata watalii milioni moja ambapo huliingizia Taifa pato la asilimia kumi na saba kiasi ambacho ni kidogo ukilinganisha navivutio vilivyopo nchini Tanzania.

  Kwapitia utalii serekali inaweza kuingiza fedha nyingi sana  pia inaweza kuwaajiri vijana wengi sana  ,iwapo ikijipanga  vizuri  na kutumia fursa vizuri kama nchi zingine  serekali yetu itaweza iwapo  itaajiri wafanyakazi ambao wanauchungu na Nchi pamoja na hifadhi zetu,pamoja na kuwa na wanataaluma wa  kutosha kuhusiana na utalii na sio kuajiri watu ambao hawana taaluma ,na siyo kuwaajiri watu kiundugu undugu na kiubinamu.

“unajua ukiona bidhaa aina soko unatakiwa uishushe bei na uangalie nini cha kuboresha ili uweze kuuza bidhaa yako sasa hapa kwetu viongozi wanapandisha bei kila siku hawaangalii chakufanya ili utalii na watalii waje kwa wingi  hapa nchini ,badala yake wanapandishi kila kitu sasa kibaya zaidi hata bei za ndege ambazo zinaleta wageni  zikitaka kutua hapa kuleta watalii wanapangiwa garama kubwa mno kiasi kwamba wanashindwa kuja, inabidi waende katika nchi jirani ya Kenya wakatue maana wenzetu wanatambua umuhimu wa kushusha bei ,na ukilinganisha Tanzania tuna vivutio vingi tofauti na nchi ya Kenya inajulikana zaidi kuliko Tanzania. “alisema Olemeiseyeki

Kwa upande afisa usiano wa chama cha waajiri  (ATE) Patricia Chao alisema kuwa maonyesho ni mazuri  na  kwani mwamko upo kwani watu wameuthuria tofauti na kipindi kingine  kwani amewaona washiriki wengi kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Kenya ,Uganda ,Rwanda ,Burundi na hata Afrika ya Kusini tofauti na kipindi kingine.




No comments