Wabunge EAC watangaza kumuunga mkono Rais Magufuli,waomba kukutana nae
.
Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (Eala), Shy-Rose
Bhanji.PICHA|MAKTABA.
NA VERO IGNATUS ARUSHA
Mbunge Shyrose Bhanji wa Tanzania, alisema kasi ya Rais Magufuli, imekuwa na manufaa makubwa sio kwa watanzania bali kwa wananchi wote wa jumuiya ya Afrika ya Mashariki.
"vita dhidi ya rushwa na ufisadi ambayo imeanzishwa na Rais Magufuli, ambaye pia ni mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, inapaswa kuungwa mkono na bunge hilo"alisema
Mbunge Martin Ngoga wa Rwanda, alisema kasi ya Rais Magufuli ambaye ni mwenyekitiwa jumuiya hiyo,inapaswa kuungwa mkono na sio vibaya jumuiya ya Afrika ya Mashariki, kuonesha kwa dhati inapambana na rushwa.
"Rais Magufuli anafanyakazi nzuri sana na sisi kama wabunge tunamuuunga mkono ili kuwa na manufaa katika jumuiya ya Afrika ya Mashariki mataifa yote yanapaswa kushirikiana kuondoa rushwa"alisema

No comments