Msanii Young Dee amewaomba Watanzania msamaha kwa kuonesha vitendo vya utovu wa Nidhamu



Rapa kiwango Bongo, Young Dar es salaam Young Dee, amewaomba Watanzania msamaha kwa kuonesha vitendo vya utovu wa Nidhamu vilivyompelekea kuingia katika matumizi ya Madawa ya Kulevya hivi karibuni.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Mapema leo jijini Dar es Salaam, msanii huyo amedai kuwa hataki kumlaumu yeyote katika mazingira ya vitendo vibaya alivyokuwa ameloeya kwa muda, bali ameamua kubadilika hivyo kuwataka wapenzi na mashabiki zake kumuunga mkono. “Sitaki kumlaumu yeyote katika hili, najilaumu mimi kujihusisha na makundi na marafiki wabaya, nlianza kutumia Pombe, sigara mpaka Madawa, hivyo nawaomba radhi Watanzania, jamii na wote niliowakwaza kwa tabia zangu, nimebadilika na kitakacho fuatia kwa sasa ni kazi nzuri kutoka kwangu” Alisema.

Katika hatua nyingine Young Dee aliweka wazi kwamba ametumia Madawa ya kulevya kwa kipindi cha mwaka mmoja na Miezi minne





No comments