Mpango wa chakula Muhimbili wasitishwa
Ule mpango wa kuwauzia chakula kwa Sh6,000 kwa siku wagonjwa
wanaolazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili umesitishwa kwa muda.
Mpango huo umesitishwa leo na Waziri Afya, Ummy Mwalimu akisema inabidi
Serikali ijiridhishe jinsi mpango huo utakavyotekelezwa.
Amesema wizara imebaini kwamba wananchi hawakushirikishwa vyema, hivyo
ameagiza uongozi wa hospitali hiyo kuanza kutoa elimu kwa wananchi ili
waelewe mpango huo.
“Ni mpango mzuri tumeukubali kama wizara, lakini tunaona kuna mambo
ambayo tunapaswa kujiridhisha kwanza, kama wagonjwa ambao wanatibiwa
kwa bima ya afya huku MNH wakihitaji kulipwa fedha taslimu kwa huduma hiyo" amesema
No comments