Ibuprofen inaweza kupunguza makali ya Ebola
Dawa ya maumivu Ibuprofen na dawa ya kutibu saratani Toremifene zinaweza
kukata makali ya virusi vya ugonjwa wa Ebola ,watafiti wamesema.
Wanasayansi walitumia Kifaa cha Diamond Light Source kuvifanya uchanganuzi
virusi vya ebola kwa kina.
Walibaini kwamba dawa hizo mbili zinaweza kushirikiana kukabiliana na Ebola
wakati virusi hivyo vinapojiandaa kuambukiza seli za mwili wa bindamu.
Hatahivyo ,watafiti hao wameonya kwamba huo ni mwanzo na kwamba dawa
zaidi zilizo na uwezo mkubwa zinafaa kutafutwa.
Synchrotron hiyo huchochea kasi ya elektroni hadi kuzalisha mwanga mkali
sana.
Hii inaweza kutumika kwa kuchambua mradi wa kutengeza vitu wa atomiki
katika mpango mkubwa zaidi kuliko darubini za kawaida.
Lengo la utafiti huo ni protini kwenye uso wa virusi vya Ebola ambayo
inaviruhusu kuambukiza seli.
''Hili ndio lengo kuu katika uso wa virusi hivyo,hili ndio huwajibika kujiweka
katika seli ,ni protini muhimu kuelewa'',alisema mtafiti Prof Dave Stuart, kutoka
Chuo Kikuu cha Oxford.

No comments