MSHAMA:ENEO LA LULANZI LISIENDELEZWE KWANZA.

| Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Asumpter Kibaha. |
MKUU wa wilaya ya Kibaha mkoani Pwani Asumpter
Mshama amewataka wananchi walioko kwenye eneo la Lulanzi wilayani maarufu kama
Matunda kutoendeleza eneo hilo hadi pale atapoomba Rais ababidlishe matumizi
kutoka viwanda hadi makazi.
Ameyasema hayo mjini Kibaha alipofanya mkutano na
wananchi walio kwenye eneo hilo ambalo awali lilitengwa kwa ajili ya viwanda
lakini lilirudishwa kwa Halmashauri ya Mji baada ya wamiliki kushindwa
kuendeleza kwa kujenga viwanda.
Mshama amesema kuwa kutokana na hali ambayo
ilijitokeza hapo na wananchi kujenga makazi huku Halmashauri ikiwataka waondoke
kwani matumizi yake bado hayajabadilishwa kuwa makazi ya kuishi.
“Kuwabomolea wananchi itakuwa ni kuwaonea kwani
wametumia gharama kubwa itakuwa ni kuwaonea ni vema tukamshauri Rais abadilishe
matumizi ya eneo hili na kuwa makazi kwani kwa wakati ule madhumini yalikuwa ni
hayo lakini kutokana na wamiliki kushindwa kujenga viwanda na watu tayari
washajenga ni vema tukaomba yawe makazi kuliko kubomoa,” alisema Mshama.
Amesema kuwa nyumba zilizojengwa katika eno hilo ni
150 na watu wamewekeza itakuwa siyo busara kuwabomolea kwani hata Halmashauri
ya Mji wa Kibaha ilifanya makosa kwa kuwaacha watu kujenga hadi kufikia idadi
kubwa kiasi hicho.
Aidha amewataka watu ambao wana viwanja na
hawajajenga kutokujenga au kufanya maendelezo yoyote hadi pale majibu
yatakapopatikana na wale waliojenga waendelee kusihi hapo hadi mwezi Novemba
ambapo atakuwa amewasiliana na wizara husika kuhusiana na eneo hilo
Kwa upande wake ofisa mipango miji wa Halmashauri
ya Mji Kibaha Gili Simiyu alisema kuwa eneo hilo lilipitishwa kuwa sehemu ya
viwanda tangu mwaka 1980 na hakuna mabadiliko yaliyofanyika yakufanya kuwa eneo
la makazi.
Simiyu alisema kuwa watu waliojenga hapo walijenga
kimakosa na watu waliowauzia hawakustahili kufanya hivyo kwani eneo hilo
lilikuwa ni maalumu kwa ajili ya viwanda tangu miaka ya 80 na hadi sasa bado
matumizi yake hayajabadilishwa.
Amesema kuwa baada ya mji huo kuwa Halmashauri ya
Mji Mdogo mwaka 2005 walianza kufanya mchakato wa eneo hilo kuwa kitovu cha Mji
baada ya waliopewa kwa ajili ya kuanzisha viwanda ksuhindwa kufanya hivyo ilikabidhiwa
Halmashauri ambapoviwanja 101 vina hati huku 37 vilikuwa bado havijasajiliwa na
Rais ndiye mwenye uwezo wa kutengua matumizi eneo hilo.
No comments