Godwin Mollel:Serikali iruhusu soko huria la uuzwaji madawa
Na Vero Ignatus Arusha
Licha ya kuzuka kwa sintofahamu kuhusu kuwepo kwa
uhaba wa dawa za binadamu nchini, Waziri kivuli wa Afya na Mbunge wa
Siha Godwin Mollel, ameitaka serikali iruhusu soko uria la uuzwaji wa
madawa nchini
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, ameshauri
serikali iruhusu shirika la Bohari la dawa nchini liwekewe mshindani
wake ili kuwezesha kuwepo kwa uwajibikaji na utendaji bora wa usambazaji
wa dawa nchini
Awali alisema shirika hilo licha ya kuwa linaidai serikali bado liko nyuma katika utoaji wa huduma zake
"leo si ajabu ukaandikiwa dawa na ukakosa hospitali za serikali ama kwenye phamasia, "alisema Godwin
"MSD imekuwa kero mahospitalini, vifaa tiba wanavyotoa si imara," alisema Godwin
Aidha alitaka serikali itoe majibu kwa serikali kuwa ni
kwanini nchi ya Tanzania inanunua dawa peke India na si kenya ambako ni
nchi karibu na Tanzania
Pia akifafanua juu ya ununuzi wa dawa alisema nchi ya
Tanzania imekuwa ikitegemea kununua dawa nchi ya India peke huku
ikisababisha kutumia muda mrefu kuingiza dawa nchini
"Kwanini tunaagiza dawa India na Si Kenya kama Kenya dawa hizo hizo zinapatikana , alisema Mbunge
"Tumegundua kuna ufisadi mkubwa unaofanyika nchi ya India ndio mana dawa zinanunuliwa India pekee
Pia alisema kutokana na upungufungu wa dawa nchini serikali
irudie pendekezo la kambi rasmi bungeni kuhusu kuongeza bajeti ya dawa
kutoka 6.1 bilioni hadi 295 bilioni
Katibu wa chadema Kanda ya Kaskazini Amani Golugwa, amesema
uhaba wa dawa nchini umekuwa ni kero kubwa hasa kwa Wazee ambao ndio
waathirika wakubwa wa tatizo hilo
"Tumetembelea wazee wa mkoa wa Kilimanjaro, Tanga, Arusha
na Manawa, kilio cha wazee ni dawa, wazee wakienda mahospitalini
wanaishi kupewa paracetamol, panadol na magnesium, hali ni mbaya sana,
"alisema Amani
Kutokana na kuwepo kwa changamoto ya utekelezaji wa mpango
kabambe wa Arusha" Arusha City Master plan "wilaya ya Arusha, Arumeru na
Arusha jiji wamekubali kuungana na kuwa pamoja kutekeleza mradi huo
Awali mradi huo ambao haukuwa sawa kwenye wilaya hizo
kupitia mkutano huo wa waandishi wa habari, wilaya hizo zimekubali kutoa
tofauti zao ili kuendeleza mkoa wa Arusha
Mwenyekiti wa halmashauri ya Arumeru, Wile Njau alisema
wilaya hizo zimeweka makubaliano ya pamoja kubainisha miradi ambayo
haikuwekwa kwenye mpango mji, ikiwa pia ni kuunganisha miradi hiyo
pamoja kwaajili ya maendeleo ya mkoa wa Arusha.
Pia alisema wamekubaliana kuanzisha kamati ya pamoja ya kusimamia mpango kabambe wa Arusha City Master Plan

No comments