Wabunge Burundi wapiga kura kujitoa ICC.
Wabunge nchini Burundi wamepiga kura
kujitoa katika mahakama ya kimataifa ya jinai ICC, na kushinikiza
uamuzi wa baraza la mawaziri wiki iliopita wa kukatiza ushirikiano na
mahakama hiyo iliopo The Hague-Uholanzi.
Ghasia za kisiasa zilianza April 2015 baada ya rais Pierre Nkurunzinza kuanza azma yake ya kuhudumu kwa muhula wa tatu.
Tangu hapo zaidi ya watu 400 wameuawa katika ghasi hizo na zaidi ya watu 200,000 wameyakimbia makaazi yao.
No comments