Waziri wa Umwagiliaji ,Eng.Gerson Hosea amwagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha kusimamia Matumizi ya fedha za miradi ya maji.
Mkuu
wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo,akiwa pamoja na mwenyekiti wa CCM Mkoa
wa Arusha Lekule Laiza na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha,
Hargeney Chitukulo wakimsikiliza Waziri wa Maji na Umwagiliaji
Eng.Gerson Lwege alipokuwa akitoa maelekezo juu ya miradi ya maji
iliyopo jiji Arusha.
|
Waziri
wa maji na umwagiliaji Eng.Gerson Hosea Lwenge, akizungumza na Mkuu wa
Mkoa wa Arusha,Mrisho Mashaka Gambo, alipomtembelea ofisini kwake jijini
Arusha.
|
Waziri wa maji na umwagiliaji Eng.Gerson Hosea Lwenge amemuagiza mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kusimamia matumizi ya fehdha za mfuko miradi ya maji zilizotolewa na Wizara kwaHalmashauri za mkoa wa Arusha.
Maagizo hayao yametolewa leo ofisini kwa mkuu huyo wa mkoa wa Arusha alipokuwa akipokea taarifa ya hali ya maji katika mkoa .ambapo amesema ilikuhakikisha miradi yote ya maji kwa mkoa wa Arusha inakamilika kwa wakati na wananchi wanaondokana na adha ya ukosefu wa maji.
Moja ya miradi hiyo mikubwa inayotazamiwa kunufaika na kutatua matatizo ya maji ni Wilaya Longido ambapo mradi huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 14 huku hatua za awali zilizoanzwa ni zausanifau wa michoro ambapo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 450
Mradi huo unatarajiwa kuongeza kiasi kikubwa cha upatikanaji wa maji katika wilaya ya Longido kutoka 20%ya sasa hai 80%ya mradi utakapokamilika
Hata hivyo Mhe. Gerson amemuhakikishia mkuu wa mkoa kuwa Wizara itajitahidi kutoa fedha zote ziliobakizaa miradi ya majikwa mkoa wa Arusha kwakuwa ni mkoa mkubwa na unategemewa kiuchumi.
Waziri huyo yupo mkoania Arusha kukazi kwa siku moja kwa lengo la kuhakikisha maendeleo ya miradi ya maji.
No comments