LEMA AZUA KASHESHE KWENYE UZINDUZI WA HOSPITAL YA MAMA NA MTOTO JIJINI ARUSHA.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg28bI9jXUWl1MFq1OUikl9pli0cJQ_g_GFTcyqlw_saFOmo9izAjAHwy112WLx8B5IOWDQQcTsdny-6vZCmANAPXF6IWrZ9QqHhrvDf1f0y_drU1lqrlaOZMRyMcyWeM4SqMsG-wOuhuu3/s1600/DSC01474.JPG
Baadhi ya wananchi waliohudhuria uzinduzi wa ujenzi wa hospitali ya mama na mtoto ambaye jina lake halikufahamika mara moja akimsihi mbunge Lema wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema atulize jazba shughuli hiyo ya uzinduzi iendelee na ampe mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo nafasi aendelee na hotuba yake kwa wananchi waliohudhuria.

 Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema akiwa anatulizwa na mchungaji Wilfred Mlay ,Wa kwanza kushoto ni mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akiwa anatulizwa na mfadhili wa Mradi huo ambaye ni daktari bigwa wa magonjwa ya kina mama na Mtoto Duniani Edrew Brown
 
Na.Vero Ignatus  Arusha.
 
Wakati Mzozano ukiendelea kati ya Mbunge Lema  na Mkuu wa mkoa Mrisho Gambo,umepelekea wafadhili wa ujenzi wa mradi wa Mama na Mtoto kutoa machozi  mbele ya wananchi kutokana na kitendo kilichotokea 

Awali ,Mtendaji mkuu wa mradi wa wakunga afrika ,Dr Andrew Blowin amesikitika kutokea kwa kitendo hicho kilichopelekea kuvurugika kwa uzinduzi wa ujenzi wa mradi wa hospitali ya Mama na mtoto  na kusema hakutegemea kama ingefikia hatua hiyo 


"Tulitaka siku hii iwe yenye furaha kwa Mama na Mtoto lakini tunasikitika imekuwa si siku ya baraka juu ya kuanzisha mradi huu,"alisema  Dr.Adrew

Mkuu wa mkoa kugoma kuja kwenye Uzinduzi

Uzinduzi wa mkutano ulikuwa uanze saa 4:30 asubuhi lakini Mkuu wa Mkoa Mrisho gambo alikaidi kuja na kusema hatoweza kufika kama Mbunge wa Mjini Godbless Lema atakuwepo
Kuzozana huko kulianza mpaka Mbunge Lema alipoamua kumigia katibu mkuu Kijazi na kumuambia kuhusu mkuu huyo wa mkoa kughahiri kwenda kwenye uzinduzi huo wa mradi wa mama mtoto 

Baada ya simu hiyo kupigiwa katibu mkuu ,Mkuu wa Mkoa Mrisho gambo alifika kwenye eneo la tukio saa 7 mchana na kuanza kuongea na wananchi 

Kulipoanza Mabishano

Baada ya mkuu huyo kufika na kuanza kuongea na wananchi ,Mrisho hambo alianza kuelezea kuhusu mradi huo na kusema mradi huo ulikuwa unaendeshwa na Taasisi ya Ukunga ya Afrika "Maternity Africa"na eneo ambalo lilitakiwa kujenga hospitali hiyo ya Mama na Mtoto lilitolewa na Marehemu Nyaga Mawala ,hivyo eneo hilo lilikuwa na Mawala 

Lakini ia alisema eneo hilo halikuwa na taasisi ya ARDF hivyo alitaka siasa ziache kutumika kutokana na eneo hilo linawahusika 


Lema alivyoanza kumjibu 


Kutokana na mkuu huyo kuongea hivyo ,Mbunge huyo alianza kugomba na kusema mkuu huyo anapotosha umma kwakua eneo hilo lilitolewa chini ya uzimamizi wake na ufadhili aliuangaikia yeye mwenyewe

"Mkuu wa Mkoa anaongea uongo"aache uongo ,"mimi nimeangaika kupata hili eneo na kupata ufadhili,"alisema Lema 
"Nimegundua anataka kutufifisha upinzani ,tunajua katumwa kufanya hivi na hatutakubali ,"alisema Lema 


Kuhusu mradi huo ,Mtendaji mkuu wa mradi wa Ukunga Afrika ,amesema mradi huu umepanga kuboresha huduma ya Mama na mtoto na kuhakikisha wanaumaliza ugonjwa wa Festula 
ambapo kupitia mradi huu watawezesha kutoa mafunzo ya ukunga yatatolewa kwa wanafunzi ikiwa lengo ni kupambana na matatizo ya uzazi kwa mama na mtoto kbala hajajifungua na baada ya kujifungua.

Amesema mradi  huo utagharimu kaisi cha shilingi 9 bilioni lengo ikiwa kuhakikisha maswala yatokanayo na uzazi yanatokomea Tanzania ,ambapo fedha za mradi huo zinatoka kwenye taasisi ikishirikiana na watu binafsi wanaotoa michango yao kutoka nje ya nchi .

"Tunatazamia mradi huu utatibu maelfu ya kina mama na zitakuwa bure ,pia wanatoa msaada yao ni watu waliokuwa na upendo na nchi hii ,"alisema Dr.Adrew.

No comments