Wa pili kushoto ni Mkrugenzi wa habari maalum Radio Bw. Leonard George, kwanza kushoto Mch Marandu Kulia ya Mkurugenzi ni Mch Rukiya Mwenyekiti wa Bodi Habari Maalum kulia kwake ni Mgeni Rasmi Ask: J. Laizer wa Naivera Apostolic Church, na wa kwanza kulia Mch. Orche Mgonja wa Lhu Pentekoste wakiwa anafuatilia kwa karibu kinachoendelea katika tamasha la Gospel Festival lililofanyika katika uwanja wa Shekhe Amri Abeid (stadium) Arusha.Picha na Vero Ignatus Blog.
Kwaya ya Sent James iliumgana na kwanya nyingine mbalimbali zilizohudhuria katika tamasha la Gospel Festival
Kwaya ya Watoto pamoja walimu wao Ulrik Alderblad ,pamoja na mwalimu Pokea Kamata, wakiimba katika tamasha hilo la Gospel Festival
The International
Singers Gospel Festival wakiwa wanaimba katika Tamasha hilo katika
uwanja wa Shekhe Amri Abeid Stadium uliopo Jijini Arusha.Picha na Vero Ignatus blog.
Muimbaji wa Nyimbo za Injili nchini Tanzania Helen Kijazi akiimba katika tamasha hilo la Gospel Festival katika uwanha wa Shekh Amri Abeid Stadium Jijini Arusha.Yeye anaimba muziki wa Injili wenye mahadhi ya Mwambao (taarabu)Picha na Vero Ignatus Blog
Vijana nao hawakukosekana ili kunogesha tamasha,Kijana Proches aliyeweka miwani kichwani na mwenzie Elias wakiwa na furaha pamoja na wenzao ambao majina yao hayakufahamika kwa haraka ,wakilifurahia tamasha hilo la Gospel Festival.Picha na Vero Ignatus Blog.
Watu mbalimbali kutoka ndani na nje ya Bara la Afrika waliohudhuria tamasha hilo la Gospel Festival Jijini Arusha.Picha na Vero Ignatus Blog.
Gospel HipHOP wakiongozwa na mnene Makwete wakiimba katika Tamasha hilo la Gospel Festival Uwanja wa Stadium Arusha.Picha na Vero Ignatus Blog
Na Vero Ignatus Arusha.
Tamasha
lililoandaliwa na Taasisi ya Kidini Radio Habari maalum(R.H.M) Mkoani
Arusha lijulikanalo kama (Gospel Festival) limefanyika jumapili katika
Uwanja wa Shekh Amri Abeid (Stadium)na kuhudhuriwa na waimbaji
mbalimbali wa ndani ya nchi na nje ya nchi ya Tanzania.
Akizungumza
mkurugenzi wa wa Taasisi hiyo ya kidini( R.H.M) Leornad George amesema
kuwa lengo kuu la kufanya tamasha hilo ni kuleta umoja wa makanisa na,
kwakupitia tamasha hilo itaondoa ule ugumu wa na fikra potofu kuwa
kanisa fulani ni bora kuliko jingine.
"Unajua
Mungu anatuhitaji sisi wote tumsifu yeye maana yeye ndiye Muumbaji
wetu,hakuna sababu ya wewe kupewa punzi ya uhai na Mungu kisha ukae
kimya bila hata kuinua sauti yako na kumsifu yeye,maana hata baada ya
maisha ya hapa duniani kupita bado tukifika kwawe kusifu kutaendelea
milele na milele"alisema Leonard.
Kwa
upande wake meneja wa kituo cha fm 97.7 ndugu Daniel Reuben Magulu
amesema kuwa wamewakaribisha waimbaji kutoka makanisa mbalimbali Arusha
na muitikio ulikuwa mkubwa,na amesema kupitia tamasha hilo zile tofauti
za waimbaji kujinitenga hazitakuwepo tena na wote tutakuwa ndugu wamoja
maana tunamtumikia Mungu.
"ifikie
mahali kila mmoja atambue kazi ya mwenzie bila kuwa na ubaguzi huku
kila mmoja akimuhesabu mwenzie ni bora kuliko yeye"alisisitiza Magulu.
Aidha
ameainisha waimbaji waliohudhuria ni kutoka nchi mbalimbali
duniani,Sweeden,Finland,Dermack,Ufaransa,Italia ,Canada na wenyeji
Tanzania ambapo amesema nchi nyingine za Afrika ya Mashariki Kenya
,Uganda,Rwanda,na Burundi watahudhuria tamasha lijalo kwa sasa wameona
waanze na hawa.
Magulu
amefafanua kuhusu( Gospel Festival ) kuwa ni sherehe ya mavuno ya
Injili,ametoa wito kwa makanisa yote na kusema kuwa Umoja ni nguvu
utengano ni udhaifu "Tuwe na umoja ili adui asipate nafasi"alisisitiza".
|
No comments