Wednesday, April 27, 2016 Mwanafunzi Amkaanga kortini polisi anayedaiwa kumbaka katika kibanda cha ulinzi cha benki.

Mwanafunzi wa kidato cha tatu, juzi alimkaanga askari polisi anayedaiwa
kumbaka kwa kuieleza Mahakama jinsi alivyotendewa kitendo hicho katika
kibanda cha ulinzi cha benki.

Akitoa ushahidi mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya Misungwi, Ruth
Mkisi, shahidi huyo alidai siku ya tukio askari huyo, Raphael Sixstus (30),
alimuita alipokuwa akipita karibu na Benki ya CRDB Tawi la Misungwi,
alipoitikia wito ghafla alivutiwa ndani ya kibanda hicho na kumbaka.

“Wakati akinitendea kitendo hicho, alikuwa akinitishia kisu huku akiniambia
nikipiga kelele ataniua, niliogopa nikaa kimya ingawa niliumia na kutokwa damu
nyingi sana,” alidai shahidi huyo.

Akiongozwa na Mwendasha Mashtaka wa Polisi, Doreth Mgenyi, mwanafunzi
huyo mwenye umri wa miaka 16 alidai kabla ya kumbaka, mshtakiwa huyo
alimvua nguo zote za ndani.

Awali, Mwendesha mashtaka alipokuwa akimsomea makosa mshtakiwa huyo
alidai kuwa Novemba 20, mwaka jana, akiwa eneo la lindo katika Benki ya CRBD
Tawi la Misungwi, alimbaka mwanafunzi huyo saa 1.00 usiku wakati akitoka
mashine kusaga unga katika maeneo ya Bomani.

Hakimu Mkisi aliahirisha kesi hiyo hadi leo itakapoendelea kusikilizwa kwa
upande wa mashtaka kuita mashahidi wengine. Mshtakiwa yuko nje kwa
dhamana.

No comments