Thursday, April 28, 2016 Rais Magufuli Atengua Uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TIC
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli,
ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC),
Bi. Juliet Kairuki kuanzia tarehe 24 Aprili mwaka huu.
Taarifa iliyotolewa na kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu wa Biashara na
Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda, imesema kuwa hatua hiyo imekuja baada ya rais
Dkt. Magufuli kupata taarifa kuwa Mkurugenzi huyo alikua hachukui mshahara
wa serikali tangu alipoajiriwa mwaka 2013 jambo ambalo linazua maswali
mengi.
Aidha, taarifa hiyo iliyosainiwa na Katibu Mkuu huyo imeongeza kuwa endapo
Bi. Kairuki atakuwa tayari kuendelea kufanyakazi na Serikali ya Awamu ya Tano
atapangiwa kazi nyingine. Mchakato wa kumpata Mkuregenzi mpya umeanza
mara moja.
Kwa mujibu wa Prof. Mkenda kwenye taarifa yake hiyo amesema Bw. Clifford
Katondo Tandali, atakaimu nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo hicho cha
Uwekezaji nchini TIC.
No comments