Saturday April 30,2016.KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI CHAFUNGUA MAFUNZO YA AJALI,VIFO NA MAJERUHI BARABARANI
Saturday, 30 April 2016
Kaimu kamanda kikosi cha
usalama barabarani Tanzania,Kamishna Msaidizi wa Polisi
Fortunatus Musilimu akifungua mafunzo kwa mawakili,waendesha
mashitaka na askari wapelelezi wa kesi za ajali barabarani
iliyoandaliwa na wizara ya afya,maendeleo ya jamii,jinsia,wazee na
watoto kwa kushirikiana na shirika la afya Duniani kupitia mpango
wa Bloomberg Initiative Global Road Safety,jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya mawakili,waendesha mashitaka na askari wapelelezi wa kesi za ajali
barabarani wakimsikiliza mgeni rasmi(hayupo pichani)wakati wa
ufunguzi huo.Mradi wa Bloomberg una nia ya kupunguza ajali,vifo
na majeruhi barabarani pamoja na kuweka vipaumbele kuzuia
vyanzo hatarishi vya ajali kama mwendokasi,kutovaa kofia
ngumu,kutofunga mikanda,vifaa maalum vya kuwakinga watoto
kwenye magari na ulevi.
Mwenyekiti wa kamati ya
Bloomberg Initiative Global Road Safety Tanzania,Mrakibu Msaidizi
wa Polisi Mathew Msuyale akimkaribisha mgeni rasmi(hayupo
pichani)pamoja na wadau wa mafunzo hayo.
Baadhi ya wadau na askari wapelelezi wa kesi za a halo za barabarani wakifuatilia
mada wakati wa mafunzo hayo.Nchini takwimu zinaonesha ukubwa wa
tatizo la ajali ni kubwa ambapo mwaka 2014 zilitokea ajali 14,360,vifo
3,760 na majeruhi 14,530 ukilinganisha na mwaka 2015 zilitokea ajali
8,337,vifo 3,468 na majeruhi 9,383 Wazazi nchini wametakiwa kuwakinga watoto wao wakati waendeshapo magari kwa kuhakikisha wanawafunga mikanda ili
kuwaepusha na ajali za barabarani na kudhibiti madhara yatokanayo na ajali.
Rai hiyo imetolewa leo jijini hapa na kaimu kamanda kikosi cha
usalama barabarani Tanzania,Kamishna Msaidizi wa Polisi
Fortunatus Musilimu wakati akifungua mafunzo kwa
Mawakili,Mahakimu ,Waendesha Mashitaka na Askari wapelelezi wa
kesi za ajali za barabarani,iliyoandaliwa na wizara ya afya kwa
kushirikiana na shirika la Afya Duniani (WHO) kupitia mpango wa
Bloomberg Initiative Global Road Safety.
Alisema wazazi wengi wanapokuwa wanaendesha magari
hawawafungi mikanda watoto wao na hivyo ajali inapotokea watoto
wanakuwa ni wahanga wakubwa kwa kupoteza maisha au kupata
ulemavu wa kudumu
?Wazazi mnawalindaje watoto,baba anaendesha gari,mtoto yupo
kwenye usukani anaendesha nae gari,hiyo siyo sahihi ,tuwalinde
watoto wawe salama kwa kuvaa mikanda?
Aidha, Kamanda Musilimu alisema tatizo la ajali barabarani nchini
imekua ikiongezeka kila mwaka na hii ni kutokana na wananchi
kutokuona kama ajali ni tatizo kubwa na la haraka ambalo linafanya
kuongezeka kwa vifo nchini kulinganisha na magonjwa mengine na
hivyo kupoteza nguvu kazi ya taifa kiuchumi
?Watu bado hawaoni kama ajali ni tatizo ,vifo inatokea hapohapo na
watoto wanabaki kuwa tegemezi,hizi ni changamoto hivyo
mshirikiane kubadilishana uzoefu ili muweze kutatua kesi zote
zinazowafikia na kupunguza malalamiko pamoja na kutenda
haki,alisema
Takwimu za hapa nchini kwa miaka miwili zinaonesha mwaka 2014
zilitokea ajali 14,360,vifo 3,760 na majeruhi 14,530 na mwaka 2015
zilitokea ajali 8,337,vifo 3,468 na majeruhi 9,383, hata hivyo Ripoti ya
Shirika la Afya Duniani ya mwaka 2015 zinaonesha ajali huua watu
1.25 milioni Duniani kila mwaka, watu kati ya 20 na 50 milioni
hujeruhuwa kila mwaka na hivyo asilimia 90 ya ajali hizi na vifo
hutokea katika nchi zenye uchumi wa kati na wa chini kama
Tanzania.
Kamanda Musilimu alisema kasi hii ya ajali ikiendelea hadi ifikapo
mwaka 2030,ajali itashika nafasi ya 5 kwa kusababisha vifo Duniani.
Mradi wa Bloomberg Initiatives ni mradi wa miaka mitano hapa
nchini umeanzishwa mwaka 2015 ukiwa na nia ya kuweka vipaumbele
vya kuzuia vyanzo vya ajali hatarishi kama vile mwendo
kasi,kutokuvaa kofia ngumu,kutokufunga mikanda,vifaa maalumu
vya kuwakinga watoto kwenye magari pamoja na ulevi.
No comments