Tuesday 26 Aprili 2016 Aliyekuwa mke wa Rais wa zamani Nchini Kenya Lucy Kibaki amefariki.

Lucy alifariki katika hospitali ya Bupa Cromwell mjini London. Alisafrishwa hadi
mjini Landon wiki moja iliopita kwa matibabu.

Akithibitisha kifo chake rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema kuwa kenya
imesikitishwa na kifo cha mama Lucy mke wa aliyekuwa rais wa Kenya Mwai
Kibaki.

Katika taarifa iliotumwa katika vyombo vya habari Uhuru amesema bi Lucy
amekuwa mgonjwa kwa kipindi cha mwezi mmoja.

Amesema kuwa Kenya imempoteza mwanamke aliyechangia mengi katika
maendeleo ya taifa la Kenya hususan katika vita dhidi ya ugonjwa wa ukimwi.
Rais ametuma risala za rambi rambi kwa mtangulizi wake Mwai Kibaki pamoja
na familia yake.


Aliyekuwa mke wa zamani wa Nchi ya Kenya Mama Lucy Kibaki amefariki dunia.

No comments