Friday, April 29, 2016 Mfanyabiashara Auawa gesti Kwa Kuchomwa Kisu
Mfanyabiashara wa mazao, Eliusta Peter(40), amefariki dunia baada ya
kuchomwa na kitu chenye ncha kali shingoni akiwa katika nyumba ya kulala
wageni wilayani Kilombero.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei alisema tukio hilo
lilitokea Aprili 22 baada ya wahudumu wa nyumba ya wageni ya Sayari
kubaini maiti katika chumba namba mbili.
Inadawa Aprili 20 mwanamke huyo akiwa na kijana mmoja ambaye jina lake
limehifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi, walifika kwenye nyumba hiyo na kuchukua
chumba kimoja wakisema wao ni wafanyabiashara wa mazao.
“Mwili wa marehemu uligundulika ukiwa kwenye nyumba ya kulala wageni
iitwayo Sayari chumba namba mbili saa 11 jioni na ulipochunguzwa
ikagundulika kuwa kifo kilisababishwa maumivu ya jereha,” alisema Matei.
Mwanamke huyo alikuwa na jeraha kushoto mwa bega lake lililotokana na
kuchomwa na kitu chenye ncha kali
Matei alisema kwa taarifa walizozipata bila shaka kijana aliyekuwa naye
anahusika na mauaji hayo.
Wakati huo huo, jeshi la polisi wilayani Kilosa limemkamata Rogasian Jeremia
kwa tuhuma za kumshambulia mkewe, Faustina Sizayi(25) kwa kumkatataka
kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake.
Mtuhumiwa alikamatwa akiwa anajihusisha na kazi ya ulinzi wa maduka baada
ya polisi kumsaka kwa muda mrefu na ndipo Aprili 24 alikamatwa baada ya
polisi kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema.
No comments