Aliyevumbua “Please Call Me” ashinda kesi 26 Aprili 2016
Mahakama ya Kikatiba nchini Afrika Kusini imeiamuru kampuni ya
mawasiliano ya Vodacom kumlipa mwanamume aliyebuni wazo la kutuma
ujumbe wa kumuomba apigiwe simu.
Gazeti la Sowetan la Afrika Kusini linasema mwajiri wa zamani wa Vodacom
Nkosana Makate aliambia mahakama kwamba huduma ya "please call me"
ilitokana na wazo lake.
Huduma hiyo humuwezesha anayetumia simu kutuma ujumbe bila malipo kwa
wateja wengine akiwaomba wampigie simu.
Tovuti ya Tech Central ya Afrika Kusini inasema uamuzi wa kesi hiyo, ambayo
imesikizwa tangu 10, itakuwa na athari kubwa.
Haijabainika Bw Makate atalipwa pesa ngapi na Vodacom.
Lakini awali amewahi kuambia Moneyweb kwamba uvumbuzi huo wake
ulizalishia kampuni hiyo karibu randi 70 bilioni za Afrika Kusini ($5bn; £3bn) na
alitaka alipwe 15% ya pesa hizo.
No comments