Monday 25 April 2016 UDUMAVU KWA WATOTO HALMASHAURI YA KISHAPU UPO JUU SABABU LISHE DUNI NA UKOSEFU WA ELIMU TANGAZO
TATIZO la udumavu kwa watoto chini ya
miaka mitano halmashauri ya wilaya
ya Kishapu mkoani Shinyanga limefikia
asilimia 43 ukilinganisha na kiwango cha
mkoa kuwa na asilimia hiyo, ambapo
imeelezwa kusababishwa na lishe duni
kwenye baadhi ya kaya na ukosefu wa
elimu ya lishe.
Akizungumza na waandishi wa habari
ofisini kwake jana mganga mkuu wa
wilaya hiyo dkt. Josephat Shani ,
alisema mwamko mdogo kwa jamii
jinsi ya kuwalisha watoto pamoja na
vyakula vinavyotakiwa bado ni
changamoto ambayo wanaendelea
kuifanyika kazi kwa kutoa elimu.
Alisema baadhi ya wazazi hawajui
vyakula ambayo mtoto mdogo anatakiwa
kupewa ili kuijenga afya yake na
kumkinga na magonjwa , matokeo yake
anakuwa na udumavu ambalo ni tatizo
kubwa kwa wilaya hiyo na mkoa kwa
ujumla na elimu inaendelea kutolewa na
wataalamu .
“Watoto wanaobainika kuwa
wameathirika zaidi na udumavu
wanapatiwa tiba ya vyakula dawa ili
kurudisha afya yao, pia jamii
inatakiwa kubadilika sasa waanze
kulima viazi lishe kukabiliana na tatizo
la lishe duni ambalo linasumbua
kwenye wilaya yetu”alisema Dkt. Shani.
Mganga mkuu alisema katika
kuhakikisha tatizo la udumavu
linakwisha au kupungua kwani asilimia
hiyo inalingana naya mkoa mzima,
wametenga sh 29 milion katika bajeti
ijayo fedha zitakazotumia kupambana na
tatizo hilo kwa kutoa elimu kwa jamii
ili ifahamu athari zake.
Mganga mkuu wa mkoa wa Shinyanga
dkt Ntuli Kapologwe hivi karibuni
alisema kiwango cha tatizo la utapiamlo
na udumavu katika mkoa wa Shinyanga
ni kikubwa, ambapo ni asilimia 43
huku akibainisha kuwa sababu kubwa
ya kudumaa kwa watoto ni ukosefu wa
uhakika wa chakula na umaskini katika
ngazi ya kaya.
Takwimu za kitaifa zinaonyesha kuwa
asilimia 42 ya watoto wenye umri chini
ya miaka mitano nchini Tanzania ,
wanaukuaji wa kudumaa kutokana na
lishe duni wakati wa ujauzito na
miaka miwili ya mwanzo ya uhai wao.
Alisema hali hiyo inasababisha watoto
kudumaa kimaumbile na akili na
kufanya kutomudu masomo shuleni na
hata kupunguza ufanisi wa kazi
wanapokuwa watu wazima.
No comments