Jumatatu, 25 Aprili 2016 17:53 Matamshi ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika mkutano na Rais wa Afrika Kusini


Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ambaye Jumapili aliwasili Tehran akiongoza
ujumbe wa ngazi za juu alikutana na kufanya mazungumzo na Kiongozi
Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu.

Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika
mkutano na Rais Zuma alisisitiza kuhusu udharura wa kuimarishwa ushirikiano
miongoni mwa nchi huru na zinazojitegemea duniani.

Katika kikao hicho aliashiria nukta muhimu katika uhusiano wa Iran na Afrika
Kusini. Awali ni hatua ya Iran kukata uhusiano wake mara moja na utawala wa
ubaguzi wa rangi wa Makaburu wa Afrika Kusini mara baada ya kupata ushindi
Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran na kusema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya
Iran ilikata uhusiano wake na utawala wa Kizayuni wa Israel na utawala wa
ubaguzi wa rangi wa Afrika Kusini takriban kwa wakati mmoja.
Kiongozi

Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amekumbushia nafasi muhimu ya hayati
Nelson Mandela wa Afrika Kusini katika kuanguka utawala wa ubaguzi wa rangi
nchini humo na historia yake nzuri, ya kiudugu na kimapenzi na Jamhuri ya
Kiislamu ya Iran. Nukta ya pili ambayo Kiongozi Muadhamu aliitaja ni kuwa,
mtazamo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuhusu Afrika Kusini ni mtazamo
mzuri na kubainisha kuwa, uhusiano wa Iran na Afrika Kusini ni mzuri sana.
Ameongeza kuwa, ushirikiano wa nchi hizo mbili katika jamii za kimataifa pia
unasaidia sana. Pamoja na hayo amesema, bado uwezo wa nchi hizi mbili
haujatumiwa ipasavyo kwa ajili ya kukuza mabadilishano ya kiuchumi na
kibiashara baina ya pande mbili.

Kwa upande wake Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ameishukuru Jamhuri ya
Kiislamu ya Iran kwa uungaji mkono wake kwa wananchi wa nchi yake wakati
wa mapambano na ubaguzi wa rangi na kusema kuwa, wananchi wa Afrika
Kusini kamwe hawawezi kusahau uungaji mkono huo wa taifa la Iran kwao.
Katika hali ya sasa ya mfumo wa kimataifa, nchi huru na zinazojitegemea
zinaweza kukidhi maslahi yao na hilo litategemea kiwango cha ushirikiano baina
yao katika nyuga mbali mbali. Lakini pamoja na hayo, hakuna shaka kuwa kuna
vizingiti katika njia ya ushirikiano huu. Hii ni kwa sababu madola makubwa ya
kibeberu na kiistikbari kamwe hayataafiki ushirikiano kama huo ambao ni kwa
madhara ya maslahi yao haramu.
Ni kwa sababu hii ndio baadhi ya madola makubwa kwa visingizio
visivyokubalika, yanajaribu kuweka vizingiti katika uhusiano wa nchi huru na
zinazojitegemea.
Iran na Afrika Kusini ni kati ya nchi zinazolengwa na njama hizo za madola ya
kibeberu.

Uzoefu umeonyesha kuwa, ushirikiano ni kwa maslahi ya nchi zinazojitegemea.
Moja ya misdaki za ushirikiano huo ni maingiliano mema ya Iran na Afrika
Kusini katika Harakati ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote.
Afrika Kusini kwa mtazamo wa kisiasa na kiuchumi ni moja kati ya nchi muhimu
na zenye taathira barani Afrika na inahesabiwa kuwa kati ya nchi zinazoibuka
kiuchumi. Iran kwa upande wake pia ni nchi yenye uwezo mkubwa na hadhi ya
kipekee katika uga wa kieneo na kimataifa na hivyo kushirikiana na Afrika Kusini
kunaweza kuwa fursa nzuri kwa nchi hizo mbili.
Kwa hakika tunaweza kusema matamshi ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi
ya Kiislamu na Rais wa Afrika Kusini ni ramani ya njia ya kufikiwa malengo ya
pamoja ya Tehran na Pretoria.

No comments