Friday, April 29, 2016 Bosi wa Zamani wa TRA na Wenzake Wawili Warudishwa Tena Rumande Hadi Tarehe 3 Mwezi Ujao
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo imesita kutoa
uamuzi wa kesi inayowakabili Harry Kitillya, Shose Sinare na Sioi Solomoni kwa
madai, jalada lake limeitishwa Mahakama Kuu.
Kitillya, alikuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA);
Sinare, Mkuu wa Idara ya Ushirikiano na Uwezekezaji katika Benki ya Stanbic na
Sioi, Mwanasheria wa Benki ya Stanbic.
Amilis Mchaura, Hakimu Mkazi Kisutu amesema kuwa, hana mamlaka ya
kutolea uamuzi wa kesi hiyo kutokana na jarada lake kuitishwa Mahakama Kuu
leo asubuhi.
Kutokana na hali hiyo Hakimu Mchaura amesema kwamba, kesi itatajwa tena
tarehe 12 Mei mwaka huu na watuhumiwa watarudishwa rumande.
Muda mfupi baada ya hakimu Mchaura kusema hivyo, Kitilya na wenzake
walirudishwa tena mbele ya Hakimu huyo baada ya hakimu kupata amri
kutoka kwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam
akimtaka kesi hiyo itajwe Mei 3, mwaka huu badala ya tarehe 12 Mei mwaka
huu aliyoipanga awali.
Hakimu Mchauru amesema, sababu za kupewa amri hiyo hazijui, hivyo kesi
itatajwa tena tarehe 3 Mei mwaka huu na yale yaliyozungumzwa asubuhi
yatabaki kama ilivyo.
No comments