Wakuu wa wilaya za Arusha wabebeshwa mzigo mzito.
| ||
|
Baadhi
ya Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Arusha pamoja na wadau wengine wakifuatilia Kikao
cha maandalizi na mapitio ya Bajeti.
|
|
Katibu
Tawala Msaidizi huduma za Mipango Mkoa
wa Arusha Bi. Grace Mbaruku
akiwasilisha mpango wa bajeti ya 2017/2018.
|
|
Katibu
Tawala Msaidizi Serikali za Mitaa Bi.
Susane Mnafe akiwasilisha taarifa ya changamoto za usimamizi wa Halmashauri
za Mkoa wa Arusha
|
Viongozi
wa Mkoa na Wilaya ya Arusha wakifuatilia mawasilisho ya mpango wa Bajeti ya
mwaka 2017/2018
ARUSHA
|
|
Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Arusha wameagizwa kusimamia
Halmashauri zao kujibu hoja zote zilizowasilishwa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha
2015/2016 kabla ya kufika mwisho wa juma lijalo.
Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo wakati wa Kikao cha maandalizi ya Bajeti ya mwaka 2017/2018
na mapitio ya bajeti ya nusu mwaka wa Fedha 2016/2017 kilichohusisha Halmashauri
zote za Mkoa wa Arusha na wataalam toka
Ofisi ya Mkaguzi wa hesabu za Serikali.
Akitoa Agizo hilo Mhe. Gambo alisema “Nataka kila Halmashauri
ikamilishe ujibuji wa Hoja kwa wakati na kwa majibu sahihi sio kufanya majibu
ambayo yanaibua hoja zaidi au hayajitoshelezi na kwa Halmashauri ambayo ilipata
Hati Chafu au Hati ya Mashaka kwa mwaka uliopita ianishe wataalamu waliopelekea
Halmashauri kupata Hati hizo ili waweze kuchukuliwa hatua Stahiki”.
Wakuu wa Wilaya mshiriki Kikamilifu kuhakikisha hoja zinajibiwa
ipasavyo na wale waliosababisha hoja hizo kwa kipindi cha nyuma wanachukuliwa
hatua ili kuleta nidhamu ili kuongeza umakini katika zoezi zima la ujibuji wa
Hoja alisema Gambo.
Aliongeza kuwa “Sitamueleza Mkuu wa Wilaya ambaye Halmashauri
yake itapata Hati Chafu au ya Mashaka kwa hesabu za mwaka ulioisha, Mkasimamie
Halmashauri zenu kwa nguvu zenu zote na katika hili sitamuonea mtu haya”.
Katika mapitio ya Bajeti ya inayoendelea alizitaka
Halmashauri ambazo hazijatoa asilimia kumi ya mapato yao kama mikopo kwa
vikundi vya wananwake na vijana zikatoe Fedha hizo kabla ya mwisho wa Januari
ili kuweza kuinua uchumi wa makundi haya yaliyoainishwa kwa mujibu wa Sera na
Maelekezo.
“Katika hili napenda kuwapongeza Halmashauri ya Jiji la
Arusha kwa kukamilisha utoaji wa mikopo zaidi ya Mil 600 kwa robo ya kwanza naya Pili
kwa mwaka wa Fedha 2016/2017 lakini halmashauri zingine zote hazijakamilisha
utoaji wa Mikopo inayotakiwa kwa kipindi cha nusu mwaka.”
Awali katika Kikao hicho akiwasilisha mapitio ya Bajeti 2015/2016
na Mpango wa Bajeti 2016/2017 Katibu Tawala Msaidizi huduma za Mipango Bi. Grace Mbaruku alisema Halmashauri
zote zinatakiwa kuandaa Bajeti Mpya kwa kuzingatia vipaumbele vilivyowekwa
katika muongozo wa Bajeti.
Halmashauri
haitazingatia vigezo vilivyowekwa inaweza kupelekea bajeti yao kukwama katika
ngazi za juu hivyo zingatieni vigezo kama kutenga Fedha za Lishe kwa ajili ya
kutokomeza udumavu kwa Watoto alisema Bi.
Mbaruku.
Akiwasilisha Taarifa ya Changamoto zinaowakabili katika
Usimamizi wa Halmashauri Katibu Tawala Msaidizi anayesimamia Serikali za Mitaa Bi. Susane Mnafe aliainisha
ucheleweshaji wa uwasilishaji wa Taarifa toka Halmashauri mara zinapohitajika,
kutofuata mfumo elekezi wa uwasilishaji wa Taarifa.
Aliongeza kuwa kutokua na kanzidata ya vyanzo vya mapato na
uandaaji wa Bajeti ya Halmashauri kabla ya Sheria ndogo mpya kupitishwa
huchangia kukwamisha ukusanyaji wa mapato kwa kutumia viwango vipya.
|
No comments