MAONESHO YA ZANA ZA KILIMO YAFUNGULIWA KWA MARA YA KWANZA MKOANI ARUSHA
Na Vero Ignatus .Arusha.
Maonyesho ya zana za kilimo yamefunguliwa jijini Arusha
ambapo ni mara ya kwanza yanafanyika katika viwanja vya Taasisi ya Utafiti wa
kilimo ya Seliani iliyopo mkoani hapa na kushirikisha wadau mbalimbali kutoka
ndani na nje ya Tanzania
Mgeni rasmi katika maonyesho hayo ni mkuu wa wilaya ya
Arusha Gabriel Daqarro,ambapo amesema kuwa serikali inawashukuru wadau kwa
kuupa mkoa wa Arusha heshima ya kufanyika kwa maonyesho hayo ambayo yatafanyika
kwa muda wa siku mbili hivyo amewataka wananchi wajitokeze kwa wingi katika
kujifunza teknolojia mpya za kilimo na ubunifu wa wataalamu mbalimbali .
Amewataka waonyeshaji kuangalia suala la bei kwani kwaasilimia
75-80 ya wakulima ni wakulima wadogowadogo hivyo ni vyema wakauza bidhaa zao
kwa bei nafuu ili wakulima wa hali ya chini aweze kumudu kununua bidhaa ili
waweze kuendana na kasi ya kilimo cha kisasa
Serikali kwa kushirikiana na wadau wa kilimo wanaangalia ni
kwa namna gani
wataweza kuboresha sekta hii ya kilimo kwa kutoa elimu
mbalimbali kwa wakulima ili kuepukana na kilimo duni ambacho kinasababisha hasara
kwa wakulima nchini.
Mkuu huyo wa wilaya amesema kuwa sekta ya kilimo inakabiliwa
na changamoto wa ufugaji wa kiholele amabao hupelekea uharibifu wa
mazingira,Teknolojia duni,ugumu wa kupata mitaji ya kuboresha miundombinu ya
kilimo





No comments