Ubalozi wa India Tanzania Wafungua Ofisi Mpya za Ubalozi Jijini Dar es Salaam.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akiweka jiwe la msingi la ufunguzi wa jengo jipya la Ubalozi wa India
lililopo mtaa wa Shaaban Robert jijini Dar es Salaam mbele ya Balozi wa
India Bw. Sandeep Arya .

Balozi
wa India hapa nchini Bw. Sandeep Arya akimuonesha Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan picha mbali
mbali zenye kuonyesha historia ya urafiki baina ya Tanzania na India
wakati wa ufunguzi wa jengo jipya la ubalozi wa India jijini Dar es
Salaam.

Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akihutubia wakati wa ufunguzi wa Jengo jipya la Ubalozi wa India hapa
nchini
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akihutubia wakati wa ufunguzi wa Jengo jipya la Ubalozi wa India
lililopo mtaa wa Shaaban Robert jijini Dar es Salaam
Balozi wa India hapa nchini Bw. Sandeep Arya akihutubia wakati wa uzinduzi wa Jengo jipya la Ubalozi wa India hapa nchini

Vikundi vya Utamaduni wa Kihindi vikionyesha uwezo wa kuzicheza ngoma za asili.
Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa India na viongozi mbalimbali na wasanii wa muziki.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassana ameishukuru Serikali ya India kwa ufadhili wake wa miradi ya maji katika miji 17 nchi ambayo inalenga kupunguza tatizo la maji kwa wananchi wengi nchini.
Makamu
wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo Jijini Dar es Salaam
katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 68 ya Siku ya Kitaifa ya Jamhuri
ya India sherehe ambazo zimeambatana na Uzinduzi rasmi wa majengo ya
ofisi mpya ya Ubalozi wa India hapa nchini.
Makamu
wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema ufadhili wa miradi ya Maji
pamoja na miradi mingine unaofanywa na Serikali ya India kwa Tanzania
Bara na Zanzibar unadhihirisha wazi mahusiano mazuri yaliyopo
yaliyoasisiwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mahatma Gandhi wa
India.
Makamu
wa Rais amesisitiza kuwa India ni moja ya washirika muhimu katika
juhudi za kuwaletea wananchi maendeleo na Serikali itaendelea kufanya
kazi kwa karibu katika maeneo mengi ikiwemo ya kikanda na kimataifa kwa
ajili ya manufaa ya wananchi wa pande Mbili yaani Tanzania na India.
Amesema
kwa miaka mingi sasa mahusiano ya kindugu yamekuwa yaakiimarika katika
sekta mbalimbali ikiwemo kisiasa,kidiplomasia,kibiashar a, masuala ulinzi, utamaduni na mwingiliano wa watu na watu.
Makamu
wa Rais pia ameishukuru Serikali ya India kwa msaada wake wa shilingi
milioni 500 alioutoa kwa wananchi wa Mkoa wa Kagera ambao walikubwa na
tetemeko la ardhi mwaka jana.
Ameeleza
kuwa Mahusiano kati ya India na Tanzania yamekuwa na manufaa makubwa
ambapo idadi kubwa ya watanzania wanaenda kupata mafunzo mbalimbali
nchini India hasa Madaktari na wamekuwa msaada mkubwa katika kuokoa
maisha ya Watanzania.
Katika
hafla hiyo, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan kwenye hotuba yake
alitoa salamu za rambirambi kwa Serikali ya India kufuatia ajali ya
treni iliyotokea katika Jimbo la Andhra Pradesh na kusababisha vifo vya
watu 30 na kujeruhi wengine.
“Kwa
niaba ya Serikali na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
napenda kutoka salamu za Pole kwa familia za wafiwa na majeruhi katika
kipindi hiki kigumu kwa kumwomba Mwenyezi Mungu azipumzishe roho za
marehemu mahali pema peponi na tunawaombea majeruhi wapone haraka. ’’
Kwa upande wake,
Balozi wa India hapa nchini Sandeep Arya amemhakikishia Makamu wa Rais
Samia Suluhu Hassan kuwa Serikali ya India itaendelea kudumisha na
kuendeleza mahusiano mazuri yaliyopo kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa
pande zote Mbili.

No comments