WATU 14 WAFUKIWA NA KIFUSI CHA UDONGO WAKICHIMBA MADINI MKOANI GEITA
WATU kumi na nne akiwemo raia wa China wamefukiwa na udongo usiku wa
kuamkia leo majira ya saa saba usiku (7:00) wakiwa wanaendelea na
majukumu yao ya uchimbaji madini kwenye kampuni ya RZ iliyopo kijiji
cha Nyarugusu Mkoa wa Geita.
Inaelezwa kuwa sababu za kuporomoka udongo ni kutokana na mgodi
kuchimbwa zamani na Wajerumani hivyo kupelekea baadhi ya maeneo hayo
kuwa na nyufa na vyuma kushindwa kushikilia udongo wa juu hali ambayo
imepelekea kuzidiwa na hatimaye kuporomoka.
Kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Geita,ikiongozwa na mkuu wa Mkoa
huo Meja jenerali mstaafu Ezekiel Kyunga imefika katika Mgodi wa RZ
kuangalia na kujionea zoezi la ukoaji .
Kamisha msaidizi wa madini kanda ya ziwa victoria Mhandisi Yahaya
Samamba ,ameeleza kuwa jitihada ambazo zimefanyika ni kuwasiliana na
migodi iliyopo karibu na eneo hilo na pia wameshaomba msaada kutoka
Kahama na kwenye mgodi wa GGM kupatiwa vifaa vya uokoaji ili zoezi hilo
liweze kufanikiwa kwa urahisi zaidi.
“Jitihada ambazo tumezifanya hadi sasa tumeomba msaada Kahama na kwenye
mgodi wa Geita,kupatiwa vifaa ambavyo vitasaidia kwa wepesi zoezi hili
la uokoaji ingawa tumeshapata vifaa vingine kutoka kwenye mgodi wa
Busolwa”,alisema Samamba.
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji Mkoa wa Geita Elisa
Mugisha,amesema eneo la chini ambalo limefukiwa na udongo ndiyo ambalo
kwa sasa wanaendelea kulitanua ili sehemu hiyo iwe kubwa watu waweze
kupita.
“Eneo lote lile la chini limefukiwa na udongo lakini kule chini
kunaonekana kuna sehemu za kwenda pembeni ingawa limefukiwa lakini chini
kuna uimara kuna uwezekano kule chini wale watu wapo hai na
wamepelekewa mipira ya hewa na kazi inayofanyika ni kutanua eneo ambalo
litasaidia kuwatoa watu hao",amesema.
Mwanasheria na msemaji wa kampuni ya uchimbaji dhahabu ya RZ Frances
Kiganga ameelezea kuwa chanzo kikubwa ni mashimo ya zamani kwani udongo
unapotikisika umekuwa ukisababisha baadhi ya nyufa kuendelea kupata
shida.
Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo Charles Julius Na Robert Stanley
ambao wameeleza kuwa mida ya saa saba usiku duara lilinza kushuka
taratibu na baada ya hatari hiyo walipewa taarifa ya watu ambao walikuwa
chini kupandisha juu lakini hata hivyo jitihada hizo hazikuzaa matunda.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga amewataka wanaosimamia zoezi la uokoaji kuongeza nguvu ya uokoaji.
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoa wa Geita Elisa
Mugisha,akitoa maelezo namna ambavyo wanaendelea na jitihada za kuokoa
Kamisha msaidizi wa madini kanda ya ziwa victoria Mhandisi Yahaya
Samamba ,akifafanua namna ambavyo wameweza kuwasiliana na makampuni
mengine ya uchimbaji wa madini kwa ajili ya kutoa msaada kwa watu
waliofukiwa
Moja kati ya wafanyakazi kwenye mgodi huo akielezea hali ilivyotokea na shimo lilivyojifukia
Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga,akiambatana
na msemaji wa mgodi huo Frances Kiganga pamoja na kamanda wa
zimamoto,Elisha Mugisha wakielekea kwenye eneo ambalo shimo
limejifukia.
Eneo la shimo likiendelea kuchimbwa
Jitihada za uokoaji zikiendelea
Baadhi ya waokoaji
Shughuli zikiendelea
No comments