WAJUMBE 14 WA BODI YA KIWANDA CHA MAZIWA CHA AYALABE WAFIKISHWA MAHAKAMANI
Na. Vero Ignatus ,Arusha
Wajumbe 14 wa bodi ya kiwanda cha maziwa cha Ayalabe na Saccos willaya ya Karatu wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha zaidi ya shilingi za Kitanzania 607milioni
Wajumbe 14 wa bodi ya kiwanda cha maziwa cha Ayalabe na Saccos willaya ya Karatu wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha zaidi ya shilingi za Kitanzania 607milioni
Wakisomewa
mashtaka mbele ya hakimu mkazi mkoa wa Arusha Doroth Msofe pamoja na waendesha
mashtaka ,mawakili wa serikali waandamizi Agnessna Halili Nuda,wakati huo
washtakiwa wakiwakilishwa na mawakili wasomi Gwankisa Sambo,na mwenzake .
Hakimu
aliyekuwa aliyekuwa anaisikiliza kesi hiyo alisema kuwa washtakiwa hawaruhusiwi kujibu chochote kwa kuwa mahakama
yake haina uwezo,
Naye
wakili msomi upande wa jamhuri Agness alisema kuwa mahakama hiyo haiwezi
kuruhusu dhamana hadi hapo Watakapata mwongozo wa kisheria kutoka kwa
mkurugenzi wa mashtaka , mahakama hiyo
itapata mwongozo kutoka mahakama ya juu (High court)
Ameyataja majina ya watuhumiwa hao Yuda Morata Male ,Anastazia Morata,Eustela Kastuli Hhyrang,Tarsila Ninah Sule,Ludovic Hunki Marmo,Maria Lohai,Suleiman Mohamed ,Everist Kwaslema,Israel Sarwat, Lazaro Titu, Florence Nesto,Constancy Nina,Saimon Philip, Zulpher Aban,Mohamed Issa ,Dickson Charles
Watuhumiwa wote 14 wamepelekwa gereza kuu la Arusha hadi tarehe 9 februari 2017.
Watuhumiwa wote 14 wamepelekwa gereza kuu la Arusha hadi tarehe 9 februari 2017.
No comments