ZIARA YA WAZIRI MKUU KASSIMU MAJALIWA JIJINI ARUSHA



 

         

          JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS
TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
HALMASHAURI YA JIJI ARUSHA
Mkurugenzi wa Jiji
Simu:

Nukushi:
+255 27 2508073/2503494 (Director)
+255 27 2544330 (General)
+255 27 2545768
S. L. P.  3013,
20 Barabara ya Boma,
23101 ARUSHA,
Barua Pepe:  cd@arushacc.go.tz
Tovuti:  www.arushacc.go.tz







TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania MHE. KASSIMU MAJALIWA wakati wa ziara yake Mkoani hapa atatembelea Jiji la Arusha kuanzia tarehe 01-03/12/2016 na kukagua miradi ya maendeleo, kuongea na watumishi wa Jiji, kukutana na wafanyabiashara pamoja na kuzungumza na wananchi wa Jiji la Arusha.

Kupitia ziara hiyo tarehe 01/12/2016 Waziri mkuu MHE. KASSIMU MAJALIWA atatembelea Kiwanda cha National Milling Company (NMC) na pia atakagua ujenzi wa barabara ya Friends Corner - Muriet yenye urefu wa Km 7 inayojengwa kwa kiwango cha Lami kupitia mradi wa Mpango Mji Mkakati (TSCP) na kusimamiwa na Ofisi ya Rais Tamisemi.

Aidha siku ya tarehe 02/12/2016 Waziri Mkuu MHE. KASIMU MAJALIWA atakutana na kuzungumza na watumishi pamoja walimu katika Ukumbi wa AICC Arusha na baadae atakutana na wafanyabiashara katika Ukumbi huo.

Hata hivyo katika siku ya tatu ya ziara yake MHE. KASSIMU MAJALIWA atatembelea na kukagua viwanda vya Lodhia pamoja na Hans Paul vilivyoko mtaa wa Viwanda – Njiro na baadae atakutana na wanachi wote kwenye Mkutano wa hadahara utakaofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid kuanzia saa nane mchana.

IMETOLEWA NA;                                   
Nteghenjwa Hosseah
Afisa Habari, Halmashauri ya Jiji
Arusha.
30 Novemba, 2016

No comments