Magufuli awataka Watanzania kufanya kazi kwa bidii
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa
na Mke wake Mama Janeth Magufuli wakiwa katika Misa ya Krismasi katika
Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida.
Hapa wakiwa katika sala.
Rais Magufuli na mkewe wakisilkiliza neno
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwasalimia waumini wa Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida mara baada ya kushiriki Misa ya Krismasi katika kanisa hilo mkoani Singida

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia waumini wa Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida mara baada ya kushiriki Misa ya Krismasi katika kanisa hilo mkoani Singida.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Baba Askofu wa Jimbo la Singida Askofu Edward Mapunda mara baada ya Ibada ya Krismasi katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Baba Askofu wa Jimbo la Singida Askofu Edward Mapunda mara baada ya Ibada ya Krismasi katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida.

Baba Askofu wa Jimbo la Singida Askofu Edward Mapunda akimuombea na kumbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya Ibada ya Krismasi katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli wakisalimiana na waumini wa Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida mara baada ya ibada ya Krismasi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli wakipunga mkono wakati wakitoka kwenye Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida. PICHA NA IKULU
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli
Rais Magufuli ametoa rai hiyo (jana) katika Kanisa la Parokia ya
Moyo Mtakatifu wa Yesu mjini Singida katika kuadhimisha Sikukuu ya
Krismasi ambayo ni kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo.
“Katika kipindi cha maisha yake Yesu Kristo hapa duniani, mbali ya
kwamba alizaliwa na mfanyakazi, Joseph seremala, lakini na yeye
alishiriki katika kufanya kazi, basi niwaombe watanzania wote tuchape
kazi kwelikweli kwa sababu hakuna cha bure,” alisema Rais Magufuli.
Pia amewataka watanzania kuimarisha upendo, kuvumiliana, na
kutobaguana, kwani upendo utalisaidia taifa kupata maendeleo huku
akiwakumbusha waumini kuwa Yesu Kristo hakuwa CHADEMA wala CCM bali
alikuwa ni wa watu wote.
Rais Magufuli ambaye aliambatana na mkewe Mama Janeth Magufuli,
katika ibada hiyo amesema, kusali ni moja ya nguzo muhimu ambayo
Wakristo wote wanapaswa kutekeleza ili kuhakikisha taifa linaendelea
kubakia katika hali ya amani na utulivu ambayo ndiyo msingi wa
maendeleo.
Aidha, Rais Magufuli ametumia fursa hiyo kuwakumbusha wakulima kote
nchini kuhakikisha wanazitumia vizuri mvua za sasa katika shughuli za
kilimo pamoja na kulima mazao yanayostahimili ukame.
No comments