RAIS MAGUFULI AONGOZA MAELFU KTK SHEREHE ZA MIAKA 55 YA UHURU WA TANZANIA BARA:ASEMA RUSHWA NI KANSA
![]() |
Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akiwa
amesimama wakati wimbo wa Taifa ulipokuwa ukipigwa uwanjani hapo.
|
![]() |
| Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akikagua gwaride. |
![]() |
Vikosi
mbalimbali vya Majeshi vikipita mbele ya mgeni Rasmi kwa mwendo wa pole na
Haraka katika sherehe za miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania Bara katika uwanja wa
Uhuru jijini Dar es Salaam.
|
Na.Vero Ignatus,Dar es salaam
Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli
amewaongoza watanzania katika kusheherekea maadhimisho ya miaka 55 ya uhuru wa
Tanzani katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es
salaam
Dkt Magufuli amesema kuwa siku hii ni siku muhimu sana katika
Taifa la Tanzania, amesema ni vyema kuwakumbuka waanziilishi wa chama
cha Tanu wakiongozwa na hayatiBaba wa Taifa mwalimu Julius Kambarage Nyerere waliojitoa kwa
hiari yao wenyewe kuutafuta uhuru wa Tanzania.
Rais amesema changamoto kubwa waliyonayo serikali ni umaskini,pamoja
na wala rushwa ambao serikali
inajitahidi kuitatua,huku akisema kuwa hatasita kuwatumbua hadharani waliozowea
kutumbua mali za watanzania hadharani,na wananchi mtambue kuwa rushwa ni KANSA
“ Katika
kuadhimisha miaka 55 ya uhuru Tanzania tumepata mafanikio makubwa tumelinda
uhuru wa nchi yetu,mipakani,tunafanya mambo yetu wenyewe,Amani na umoja pamoja
na mshikamano,na Watanzana wamebakia kuwa wamoja ,hatubaguani rangi, imepiga
hatua katika maeneo mbalimbali ikiwemo ujenzi wa barabara za
kisasa,madaraja,vivuko,meli,viwanja vya ndege na miradi ya maendeleo n.k”amesema
Magufuli.
Aidha rais amesema kuwa pamoja na kuhakikisha taifa linabana
matumizi bado imegundulika kuwa wapo wafanyakazi hewa 19,000,kwenye mradi wa
Tasaf zipo kaya masikini hewa 55,000 na wanafunzi hewa 65,000 ,”sintalifumbia
macho kwani juhudi zote hizi ni kwaanjili ya kuboresha maslahi ya watanzania wote na siyo
mtu binafsi “alisema Magufuli.
Amewaomba Watanzania waendelee kudumisha Amani,mshikamano na
waendelee kuulinda Muungano wa Tanzania,huku akiwatakata Watanzania waendelee
kuchapa kazi kwa bidii .”kama falsafa yetu inavyosema’ hapa kazi tu’ huku wakijua kuwa hakuna babu,bibi,shangazi,wala
mjomba wa kuiletea maendeleo nchi hii ya Tanzania ila sisi wenyewe”alisisitiza rais.
Wakati huohuo Dkt Magufuli amesema sherehe za maadhimisho ya miaka 56 ya uhuru mwaka 2017 yatafanyika makao makuu ya nchi Dodoma na kusisistiza kuwa kwa jiji la Dar es salaam itakuwa ndiyo ya mara ya mwisho haya ya miaka 55 ya 2016.
Wakati huohuo Dkt Magufuli amesema sherehe za maadhimisho ya miaka 56 ya uhuru mwaka 2017 yatafanyika makao makuu ya nchi Dodoma na kusisistiza kuwa kwa jiji la Dar es salaam itakuwa ndiyo ya mara ya mwisho haya ya miaka 55 ya 2016.









No comments