RAIS MAGUFULI AZIAGIZA HALMASHAURI ZOTE NCHINI KABLA YA MWISHO WA MWEZI HUU WAWE TAYARI WAMENUNUA DAWA ZA VIUAWADUDU WA MALARIA

 
Na.Vero Ignatus Kibaha,Pwani
 
Rais Dkt.Magufuli amefanya ziara katika kiwanda cha kutengeneza dawa za kuulia vimelea vya mbu wanaosababisha malaria kilichopo Kibaha, Pwani.

  Katika ziara katika kiwanda hicho ametoa siku 10 kwa Halmashauri zote nchini kwenda kuchukua dawa za kuua wadudu wa malaria wanaokuwa kwenye maji yaliyotuama na kupulizia katika maeneo ya makazi ya watu
 
"Nataka tatizo la watanzania kuugua malaria liishe kabisha nataka nione wagonjwa wamepungua hospitalini ,na nyie wenye kiwanda tengenezeni madawa yenye kiwango,naomba kiwanda kifanyae kazi na wafanyakazi walipwe mishahara yao."alisema Magufuli  

 Awali, Kaimu Meneja wa kiwanda hicho, Samweli Mziray alimweleza Rais kuwa dawa takribani lita 100,000 zipo tu kiwandani hapo baada ya wanunuzi wakuuu ambao ni Halmashauri za Wilaya kushindwa kuzinunua kwa madai ya kukosa fedha ambapo lita moja ya dawa hiyo inauza shilingi 13,200
 
Kadhalika, Rais ameiagiza Wizara ya Fedha kutoa Sh1.3 bilioni  kwa ajili ya kulipia dawa  hizo za kuua vimelea vya mbu zilizopo katika kiwanda ambapo ametoa wiki moja fedha hizo ziwe zimeshawasilishwa kiwandani hapo.

“Sasa mimi nimeshatoa agizo dawa zilipiwe, sasa nione mkurugenzi ambaye atashindwa kutekeleza agizo langu la kufata dawa hizo kwa kipindi nilichotoa, nimesema natoa muda mpaka  mwisho wa mwezi, "amesema Rais Magufuli.
 
Rais amesema kuwa Watanzania wapo tayari kwenda kununua madawa nje ya nchi kwa gharama kubwa wakati hapa nchini kuna kiwanda kipo na kinatengeneza dawa ya kuua viluilui vya malaria.
 
"Kiwanda kimekuwa tayari watanzania hawataki kununua dawa."alisema

 

No comments