Rais aagiza walioshindwa kuendeleza viwanda wakamatwe, wawekwe gerezani,Watanzania walioweka fedha zao nje ya nchi waje wawekeze kwenye viwanda


Na.Vero Ignatus ,Chalinze Pwani.

Rais John Magufuli amemwagiza Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage, kuwanyang’anya viwanda wamiliki ambao wameshindwa kuviendeleza.

Ameyasema hayo katika siku yake ya mwisho wa  ziara yake ya siku tatu mkoani Pwani ambapo alikwenda kuzindua kiwanda cha Sayona kilichopo  Mboga halmashauri ya chalinze ambapo amemuagiza waziri kuwafuatilia wale wote waliouziwa viwanda na hawajaviendeeza kuwanyang’anya na kuwapa wawekezaji wengine ambao wanaweza kuviendeleza.

 “Viwanda siyo mwanamwali wa kutunzwa ndani ,waziri nakuagiza tumia nguvu katika kufuatilia hili, nataka siku moja uniletee orodha watakaojifanya wajuaji wa kupinga niambie tutatumia hata polisi kuwakamata na kuwasondeka ndani”.alisema Rais.

Kutokana na hilo, Rais amesema; "natoa wito kwa wote waliouziwa viwanda kipindi cha nyuma na sasa wameshindwa kuviendeleza , naagiza sasa basi mrudishe  na wewe Waziri Mwijage tumia hata nguvu kama kuwaweka ndani weka tu siku akitoka huko atakuta kiwanda kimeanza kazi."

“Kipindi cha nyuma tulipofanya makosa ni pale tulipouza viwanda kwa watu binafsi, sasa  kuna  viwanda 197 vimeshakufa waliouziwa hawajishughulishi na vingine vipo kama magofu,” amesema.
“Watanzania wote walioweka pesa zao nje ya nchi waje wawekeze kwenye viwanda hapa nchini kwani wakifa na fedha zao zitakufa vilevile,makosa tuliyoyafanya ni kuuza viwanda kwa watu ambao wameshindwa kuviendeleza mfano morogoro kunawatu wanafugia mbuzi kwenye majengo ya vilivyokuwa viwanda ni aibu kubwa.”alisema


No comments