AJALI YA MAGARI MAWILI ,PIKIPIKI YAUA WATU SABA MOSHI,YUMO MWANDISHI WA HABARI NA MWENYEKITI WA CCM


ajali ccm
WATU saba wamepoteaza maisha papo hapo katika tukio la ajali ya barabarani iliyotokea leo jioni Jumapili February 5,2017 katika eneo la Mwika mpakani mwa Wilaya ya Rombo na Moshi Vijijini Mkoani Kilimanjaro.

Waliopoteza maisha ni pamoja na Mwandishi wa gazeti la Habarileo ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Hai, Anorld Swai.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,SACP,Wilbroad Mutafungwa alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa ajali ilitokea majira ya saa 11 jioni ikihusisha magari mawili na pikipiki maarufu kama Bodaboda.

“Ajali imetokea majira ya saa 11 jioni ambapo watu saba wamepoteza maisha wanne ni kutoka katika Toyota Surf T606 AQZ, mmoja katika bodaboda MC 101 ANC huku wengine wakiwa ni kwenye Fuso T343 BNL,”alisema Kamanda Mutafungwa.

Alisema ajali hiyo ilitokea katika eneo la Mwika katika Kijiji cha Mawanjeni katika mpaka wa Wilaya ya Rombo na Wilaya ya Moshi Vijijini na kusema kuwa chanzo cha ajali hiyo inaweza kuwa ni kuharibika kwa mfumo wa Breki wa Fuso iliyokuwa imebena ndizi ikitokea Rombo kwenda Jijini Dar es Salaam.

Mbali na Swai wenginw waliopoteza maisha na kutambulika ni Mjumbe wa NEC ya CCM na Katibu wa CWT kutoka Same Ally Mbaga, Mwenyekiti wa UWT Anastazia Malamsha, Edwin Msele, Mwanafunzi wa mwaka wanne Chuo cha KCMC.

Majeruhi wa ajali hiyo ni Jackson Kimambo - Mwandishi gazeti la Nipashe - amekimbizwa Hospitali ya KCMC kwa Matibabu pamoja na Mwendesha Bodaboda.
Anord SwaiAnord Swai enzi za uhai wake
Ujumbe Anord Swai aliotuma kwenye group la Whatsapp kabla ya kifo chake leo alasiri saa 9.20 
Marehemu Anord Swai enzi za uhai wake

ajali moshi kilimanjaro

Ajali Kilimanjaro

Picha za ajali ya mkoani Kilimanjaro

Ajali kilimanjaro

No comments