CHAMA CHA WAALIMU MKOANI ARUSHA WAMUUNGA MKONO WAZIRI MKUU
Na.Vero Ignatus ,Arusha.
Chama cha walimu mkoa wa Arusha,imeazimia
kuungana na Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa kupiga vita utumiaji na uzaji
wa viroba
Akizungumza na
waandishi wa habari mkoani hapo, Mwenyekiti wa Chama cha walimu jiji la
Arusha,Joyce Msaki amesema walimu mkoa wa Arusha wameunga mkono
jitihada za waziri mkuu juu kupambana na utumiaji wa viroba kwakua
shule pia zimeathiriwa na utumiaji wa pombe hizo
Wiki
iliyopita Waziri Mkuu Kassim Majaaliwa,akiwa kwenye ziara mkoani
Manyara alitoa tamko la kuzuia matumizi pamoja na uuzwaji wa pombe aina
ya viroba na kusema mpaka ifikapo tarehe 1 machi vinywaji hivyo viwe
haviuzwi tena
Hata hivyo
,alisema utumiaji wa pombe hizo mashuleni umesababisha nidhamu kushuka
kwa wanafunzi ikiwa baadhi ya walimu kuambuliwa kupigwa na wanafunzi
ambao wametumia pombe hizo
Pia
alisema,kutokana na urahisi wa pombe hizo ilikuwa ngumu kwao kudhibiti
hasa wanafunzi kuwa na mtindo kuchanganya kwenye maji na kwenda nazo
mashuleni
"Mtindo
uliokuwepo walikuwa wanavikata wanachanganya maji,hivyo inakuwa ngumu
kutambua utakachogundua baadae ni tabia yake baada ya kutumia,"alisema
Jocye
"Walimu mkoa wa
Arusha tunampongeza Waziri Mkuu kwa vita aliyoanzisha na tunahaidi
kupambana kwenye vita hii ili wanafunzi waweze kufanya vizuri kwenye
masomo yao,"alisema Jocye
Pia
alisema ipo sababu ya serikali kuzingatia sheria ya utengenezaji wa
pombe nchini hasa kwakusisitiza upakiaji wa pombe hizo uwe wa ujazo
mkubwa na si kwenye vifungashi vya viroba
Mwanafunzi
unakuta anapewa 1000 hadi 2000 ya nauli,kiroba kinauzwa bei 500 hadi
600, kwa bei hii ni raisi kununua lakini mfano konyagi ndogo 3500 na
kubwa 7000 kwa mwanafunzi kununua ni ngumu,bora ziuzwe ghali
iliwashindwe kununua,"alisema Jocye
Wakati
huohuo,Katibu wa Walimu jiji la Arusha,Nuruel Kavishe alisema agizo la
Waziri Mkuu litarahisisha walimu kufundisha mashuleni hasa wanafunzi
kuwa na uwezo mkubwa wa kuelewa kuliko awali ilivyokuwa
"Tunaushaidi
mkubwa kuwa kweli wanafunzi wanatumia viroba hasa wanafunzi wa shule za
sekondari,sisi tutamsaidia Waziri kupambana na vita hii
Hata
hivyo,alisema kama walimu baada ya tarehe 1 machi kufika kama viroba
vitaendelea kuuzwa ,watatoa taarifa kwa Waziri mkuu ikiwa ni pamoja na
kumpelekea majina ya wauzaji wa pombe hizo
Mwakilishi
wa walimu vijana mkoa wa Arusha Denis Lubida alisema licha ya pombe
hizo kukatazwa zitasaidia kuwepo kwa dhana ya uwajibikaji kwanzia
mwanafunzi,mzazi pamoja na walimu
Akiendelea kusema hivyo alisema pombe hizo hazikumuathiri mwanafunzi peke hata waalimu pia waliathiriwa na pombe hizo
No comments