TIGO Marathon Mtanzania Ang'ara, Huku Wakenya wakiendelea kutesa Marathon




Wa kwanza kushosto ni Katibu mkuu wa wizara ya habari ,utamaduni sanaa na michezo ,Profesa Elisante Ole Gabriel ,akiwa jukwaa kuu na mkuu wa moa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadick wakifuatilia mbio zilizokuwa zinaendelea katika uwanja wa Ushirika Picha na Vero Ignatus Blog
Mratibu wa Kili Marathon  Agrey Mariale akiweka mambo sawa uwanjani hapo .Picha na Vero Ignatus blog
Mshindi wa kwanza wa nusu Marathon kilometa 21 raia wa Tanzania Emmanuel Giniki aliyeweka tishet ya bluu begani na maji mkononi
Emmanuel Giniki akihojiwa na wandishi wa habari baada ya ushindi wake wa nusu Marathon  akiwa na namba 4446 na alikimbia saa 1:03:49 .Picha na Vero Ignatus Blog



Mshindi wa kwanza mwanamke katika mbio za kilometa 21 Grace Kimanzi kutoka nchini Kenya akiwa na namba 5874 akimalizia mbio hizo na kuibuka mshindi ambapo alikimbia kwa muda wa 01:143:06.Picha na Vero Igatus Blog.
Mshindi wa kwanza wa mbio za kilometa 42.2 Moses Hengitti kutoka nchini Kenya akiwa na namba 207ambaye alikimbia kwa muda wa saa 2:16:42.Picha na Vero Ignatus Blog
Mshindi wa pili mwanamke wa mbio za kilometa 42 Marathon Shemith Nyawira Muriuk kutoka Kenya mwenye namba 549 ambaye alikimbia kwa saa 2:43:42. Picha na Vero Ignatus Blog

Kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha Charles Mkumbo naye alishiriki mbio zaklometa 21,pichani akiwa anamalizia mbio hizo zilizofanyika Moshi mkoani Kilimanjaro Katika viwanja vya Chuo cha Ushirika.Picha na Vero Ignatus Blog.

Washiriki wakimalizia mbio zao hadi watoto wadogo wameshiriki kama wanavyoonekana pichani hapo.Picha na Vero Ignatus Blog

Miss Tanzania Miriam Odemba akiwa anamalizia mbio za kilometa 21 katika Kili Marathon iliyofanyika Moshi Mkoa wa Kilimanjaro.Picha na Vero Ignatus

Babuuuu!!  Joram Zakaria Mollel( 90)nae alishiriki kama kawaida yake miaka yote .Picha na Vero Ignatus Blog
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadick akimpongeza mzee Joram Zakaria Molell (90)ambaye alishiriki mbio za kilometa 21 Kili Marathon iliyofanyika Moshi Kilimanjaro Picha na Vero Iganatus Blog
 
Mkurugenzi wa Tigo kanda ya kaskazini George Lugata akitoa neno la shukranikwa washiriki wa Kili Marathon,pamoja na wananchi waliotoka katika mikoa tofauti pamoja na nchi mbalimbali Afrika na nchi za Ulaya walioshiriki mbio hizo.Picha na Vero Ignatus blog
Baadhi ya washiriki wa Kili Marathon wakielekea eneo la kuanzia mbio .PICHA NA VERO iGNATUS bLOG


Washiriki wa NUSU Kili marathon wakiwa tayari kwenye point ya kuanzia mbio kama wanavyoonekana pichani washiriki wa mwaka huu wa mbio hizo za kilometa 21 ni zaidi ya elfu tano.picha na Vero Ignatus Blog
Mbio zikiedelea kwa kasi hadi apatikane mshindi .Picha na Vero Ignatus Blog
Mambo ndivyo yalivyokuwa yakiendelea katika kilimarathon .Picha na Vero Ignatus BLOG









Wakimbiaji wa mbio za kilimarathon pamoja na mashabiki mbalimbali wakiwa uwanjani wakiwafurahia nndugu jamaa na marafiki wanaoendelea na mbio hizo Picha na Vero Ignatus Blog
Mbio zikiedelea kwa kasi hadi apatikane mshindi .Picha na Vero Ignatus Blog
Image may contain: one or more people, people standing and outdoor
Baadhi ya washiriki akiwemo Ramson Walter wakifurahia baada ya kumaliza mbio za kilometa 21  hapa mwenye namba 4375

Na,Vero Ignatus .Kilimanjaro

Mbio za Kili marathon zimefanyika jana manispaa ya Moshi mjini  mkoani kilimanjaro katika viwanja vya chuo cha ushirika ambapo wakimbiaji zaidi ya 8000 wameshiriki mbio hizo

Mbio hizo zimefunguliwa rasmi na Katibu mkuu wa wizara ya habari utamaduni sanaa na michezo Elisante Ole Gabriel ya saa  kumi na mbili nusu ambapo mbio za kilometa 42 zilianza, huku wale kilometa 21 wakianza mbio hizo majira ya saa moja kamili asubuhi

 Mbio hizo ziligawanyika katika makundi tofautitotauti kuna wale waliokimbia kilometa 42,km 21 km 10 ambazo zilishirikisha walemavu pamoja na zile za kilometa 5 ambapo kila kundi walipatikana washindi wa mbio hizo.

 Mshindi wa mbio za kilometa 21 ni raia  wa Tanzania Emmanuel Giniki akifuatiwa na mshindi wa pili George Waiyaki kutoka Kenya,Alexander Muyao kutoka kutoka kenya,washindi kwa upande wa wanawake kilometa 21 Grace Kimanzi kutok Kenya,Cherkemo Vicroy kutoka Kenya,Valentine Kipketer kutoka Kenya

Mshindi katika mbio za kilomita 42.2 ni raia kutoka kenya Moses Mongick, wa pili ni wilium Koskei kutoka kenya,na watatu ni Kepte Targus Kipkemoi kutoka Kenya kwa upande wa wanawake mshindi wa kwanza ni  Shemith Nyamwira Muriuk kutoka Kenya,Teresia Amosa kutoka Kenya na Aveline Atanja kutoka Kenya 

No comments