Waandamana kupinga ongezeko la bei ya petroli Mexico


  Ongezeko hilo limewakwaza wananchi walio wengi
Ongezeko hilo limewakwaza wananchi walio wengi

Mamia ya waandamanaji kutoka katika majimbo kumi na mbili nchini Mexico wameendelea na maandamano na kufunga barabara wakilalamikia ongezeko la asilimia ishirini ya bei ya mafuta ya Petrol.

Hatua hiyo iliyoanza kutumika tarehe moja Januari vimesababisha machafuko nchini humo.

Zaidi ya watu mia tano wamekamatwa na maduka mengi yamevamiwa.

 
Zaidi ya waandamanaji 250 wamekamatwa na polisi
Zaidi ya waandamanaji 250 wamekamatwa na polisi
Rais Enrique Pena Nieto amesema kuongezeka kwa bei ya petroli ilikuwa ni lazima kutokana na kuongezeka kwa bei ya mafuta duniani kote.

Wanasiasa wa upinzani wamewaasa wananchi kuwa na subira na kwamba waandamanaji wasijihusishe katika masuala ya uvamizi na vitendo vya uharibifu

No comments