Zaidi watu 250 wameuawa kwenye maporomoko ya ardhi Sierra Leone
Maporomoko ya ardhi yafukia watu wengi Sierra Leone
Idadi ya watu waliouwa kwnye maporomoko ya ardhi nchini Sierra Leone haujulikani baada ya idaia tofauti kutolewa.
Shirika la habari la AP linasema kuwa takriban watu 250 wameuawa.Eneo moja la milima liliporomoka mapema leo Jumatatu kufuatia mvua kubwa, na kusababisha nyumba nyingi kufukiwa kwa mjibu wa mwandishi wa habari wa BBC Umaru Fofana
Makamu wa rais nchini Sierra Leone Victor Bockarie Foh, alisema kuwa kuna uwezekano kuwa mamia ya watu wameuawa akiongeza kwa idadi ya watu waliouawa huenda ikaongezeka.
- Maporomoko ya ardhi yauwa 15 China 100 hawajulikani waliko
- Maporomoko ya ardhi yaua watoto 44 Colombia

"Tulikuwa ndani, tukasikia udongo ukikaribia, tukajaribu kukimbia, nilijaribu kumchukua mtoto wangu, lakini udongo ulikuja kwa haraka sana . Alifukiwa akiwa hai. Sijamuona mume wangu. Mtoto wangu alikuwa na umri wa wiki saba." alisema muathiriwa mwingine.

Watu wamesambaza picha za uharibifu uliotokea kwenye mtandao wa twitter ya za mafuriko ndani nanje ya mji wa Free town.

No comments