WANAFUNZI WA LUCKY VICENTI KUREJEA NYUMBANI KESHO IJUMAA


Balozi wa Tanzania nchini Marekani Wilson

 Pichani ni watoto Sadia,Doreen na Wilson pamoja na mama zao ,(aliyevaa suti) ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani Wilson Masilingi wakiwa sioux City Lowa nchini Marekani.Wanatarahiwa kurejea nchini siku ya ijumaa asubuhi.

Na.Vero Ignatus,Arusha
 
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwaongoza Watanzania kuwapokea majeruhi (3)wa ajali wa Shule ya Lucky Visent katika uwanja wa kimataifa wa KIA siku ya ijumaa wakitokea nchini Marekani  majira ya saa tatu asubuhi kwa ndege aina ya DC -8 namba SP ambayo imetolewa na shirika la The Samaritan Purse kutoka mji mkuu Shaloth North Carolina  na watakuwa angani kwa masaa 18.

Akizungumzia ujio wa wanafunzi hao Mbunge wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu amewaomba wazazi ndugugu jamaa na marafiki wanaopenda kuwapokea watoto hao wawahi uwanjani saa amesema kuwa ujumbe wa baraza la congress ukiongozwa na ujumbe wa baraza Man Stive King  pamoja na wageni mbalimbali  watawasili Kilimanjaro saa moja kamili asubuhi siku ya ijumaa

Aidhaa amesema kuwa watoto Doreen, Sadia na Wilson wapo tayari kurejea nyumbani ,amewaomba watanzania wajumuike pamoja kuwapokea watoto hawa .ambao walipelekwa marekani mei 14 kwaajili ya matibabu yaliyoratibiwa na Stemm kwa kushirikiana na shirika la ndege la Samaritan Purse linaloongozwa na mchungaji Franklin Graham wa nchini Marekani

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na mbunge huyo  ambae tangia watoto hao wasafirishwe amekuwa akitoa taarifa kupitia mtandao wa kijamii facebook  amesema kuwa ndege itakayowarudisha watoto hao pamoja na mama zao na daktari bingwa  Elias Mashalla na muuguzi kutoka hospitali ya Mount Meru itawasili ijumaa asubuhi.

Ikumbukwe kuwa watoto hao ni manusura wa ajali iliyotokea mei 6/ 2017  ambapo wenzao 32 walipoteza maisha ,walimu 2 na dereva mmoja ,wao  walisafirishwa kuelekea nchini Marekani na Shirika la Samaritan Purse kwaajili ya matibabu.

No comments